NA HAJI NASSOR, PEMBA
WAJASIRIAMALI wa ususi wa mikoba ya
kisasa inayotumia ukindu na kitambaa kisiwani Pemba, wamesema mafunzo ya
utengenezaji wa mikoba, waliopatiwa na Chama cha Waandishi wa habari wanawake
Tanzania TAMWA, kupitia mradi wa WEZA II, yanaweza kuwapa uhakika wa soko.
Walisema
mikoba hiyo ambayo ni tofauti na ile walioizoea, hawana wasiwasi mkubwa wa
soko, kutokana na aina hiyo kuwa mpya na haijakuwa mengi sokoni.
Wakizungumza
na mwandishi hizi kwa nyakati tofauti, walisema baada ya mafunzo hayo, sasa
kazi iliobakia mbele yao, ni kutengeneza mikoba hiyo, ili wapate njia ya
kujikwamua kiuchumi.
Mmoja
kati ya wajasiriamali hao kutoka Kiuyu, Maulid Saleh Hamad, alisema yeye mikoba
ya aina hiyo, kwake ni mipya na anaamini akishapa vifaa, hatarajii kukosa soko.
“Mikoba
ni mizuri na wala hujui kuwa ni ya ukindu, hapa TAMWA kupitia WEZA II,
imetuonyesha njia ya kufikia malengo yetu kicuhumi sisi wanawake wajasiriamali’’,alifafanua.
Nae
Time Khamis Juma kutoka Tumbe Magharibi alisema, anachoomba ni kuona TAMWA,
inawapatia cherahani za kisasa kwa ajili ya kushonea mikoba hiyo.
“Mafunzo
tayari, sasa kazi iliobakia kwa TAMWA kupitia WEZA II, kabla ya mradi
kumalizika mwaka 2019 watupatie vyerahani, ili kazi na malengo yetu yafikie
haraka’’,alieleza.
Kwa
upande wao Mafunda Faki Hamad wa Kiungoni kimango, na Zamu Khamis Saburi wa
Kengeja walikipongeza TAMWA, kutokana na kuwapatia mafunzo hayo, ambayo
walipaswa kumlipa mtaalamu fedha nyingi, ili kuwapatia mafunzo hayo.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu, mratibu wa mradi wa kuwawezesha
wanawake kiuchumi, Asha Abdi Makame kutoka TAMWA, alisema wanalo lengo la
kuwapatia wajasiriamali hao vifaa.
“Kwenye
mradi huu wa miaka mitatu, tunalo lengo la kuwanunulia vifaa wajasiriamali hao,
ikiwa ni pamoja na vyerahani, ingawa hawatoenea wote 100’’,alifafanua.
Hata
hivyo Mratibu huyo, aliwataka waliopata mafunzo hayo, kuhakikisha wanawapa na wenzao,
ili lengo la TAMWA la kuwainua wanawake kiuchumi, lifanikiwe.
Zaidi
ya wajasiriamali wanawake wa ususi wa mikoba 100 kutoka shehia 25 kisiwani
Pemba, wamepatiwa mafunzo ya ususi wa mikoba ya kisasa, inayotumia ukindu,
kitambaa, zipu na vipolo.
No comments:
Post a Comment