Idara ya Da’wah ya taasis ya The Islamic
Foundation (TIF), inafuraha kuwatangazia wanafunzi wote Waislamu waliomaliza
Kidato cha Sita (Form VI) si zaidi ya miaka mitano (5) iliyopita kwamba kuna
nafasi za masomo kwa ufadhili asilimia mia moja kwenda kusoma masomo ya DINI na
DUNIA chuo kikuu cha kiislamu madina nchini Saudi Arabia.
KOZI ZITAKAZOTOLEWA:
Kozi zitakazotolewa ni kama ifuatavyo;-
1.
Kitivo cha Sharia -Faculty of Islamic Law ()
2.
Kitovo cha Dawah -The Faculty of Islamic
Preaching (Da’wah) and Theology (Da’wah na Usuul-Diyn)
3.
Kitivo cha Qur’an - Faculty of Holy Qur’an and
Islamic Studies
4.
Kitivo cha Hadithi za Mtume - Faculty of
Prophetic Tradition and Islamic Studies
5.
Kitovi cha Lugha ya Kiarabu - Faculty of Arabic
Language
6.
Kitovo cha Sayansi - Faculty of Science (Digrii
ya Kwanza ya Hisabati, Kemia au Fizikia)
7.
Kitovo cha Kompyuta- Faculty of Computer and
Information System (Digrii ya kwanza ya Sayansi ya Computer, Information System
au Information Technology)
8.
Kitovo cha Uinjinia - Faculty of Engineering
(Digrii ya kwanza ya Civil Engineering, Electrical Engineering au Mechanical
Engineering)
MUOMBAJI AKISHAKUBALIWA ATAPATIWA YAFUATAYO BURE:
1.
Tiketi ya ndege kwenda na kurudi kila mwisho wa
mwaka wa masomo
2.
Posho ya kujikimu ya kila mwezi
3.
Posho ya ziada kwa mwanafunzi atakayefanya vizuri
sana katika masomo yake
4.
Malazi bure yenye kila kitu, kwa wanafunzi ambao
hawajaoa
5.
Chakula katika kantini ya Chuo kwa ada nafuu
6.
Huduma bora za afya katika hospitali ya chuo
7.
Usafiri bure kwenda Msikiti wa Mtume (masjid
Nabawiy) na kurudi
8.
Huduma zote za kijamii, Internet na michezo zianazotolewa
na chuo bure
MASHATI YA KUJIUNGANA CHUO
1.
Muislamu mwanamme mwenye maadili mazuri
2.
Muombaji awe na afya njema
3.
Muombaji lazima afaulu usaili na majaribio kama
yatakavyotolewa na chuo
4.
Muombaji lazima awe na Shahada ya Thaanawiy
iliyotolewa na Chuo au Ma’had inayotambuliwa
5.
Muombaji lazima awe na Cheti cha Elimu ya
Sekondari ya Juu (GCSE) au kinacholingana nacho kutoka ndani au nje ya Saudi
Arabia
6.
Cheti lazima kiwe kimetolewa na Wizara kutoka
katika shule ya serikali au shule binafsi
7.
Muombaji lazima awe tayari kusoma mfululizo
8.
Isiwe imepita zaidi ya miaka mitano (5) tangu
amalize masomo yake ya A-level GCSE
9.
Asiwe na umri zaidi ya miaka ishirini na tano
(25) wakati atakapoanza masomo yake chuoni
10. Kwa wale wanaotaka
kusoma Kitivo cha Qur’an lazima muombaji awe amehifadhi Qur’an yote au nusu
yake kwa ahadi kuwa atamalizia kuhifadhia kiwa chuoni
11. Muombaji lazima awe
tayari kutii masharti na sheria za chuo
ILI MAOMBI YAKAMILIKE, MUOMBAJI
ANATAKIWA AWE NA;-
1. Cheti cha kumaliza Elimu ya Sekondari (A
Level au GCSE)
2. Shahada ya Thaanawiy inayotambulika
3. Cheti cha kuonesha ufaulu wa muombaji
katika GCSE (A-level Transcript)
4. Ushahidi wa kuwa na tabia njema (Tazkiya) kutoka Taasisi ya
Kiislamu inayofahamika au Mwanawachuoni anayekubalika katika jamii
5. Cheti cha kuzaliwa
6. Hati ya Kusafiria (Passport) isiyokwisha
muda wake
7. Kitambulisho cha urais au Mpiga kura
8. Picha Passport Size (6x4)- Picha ipigwe nyuma ya picha
(background) nyeupe, asivae miwani wal akufumika kichwa (kichwa wazi)
9. Hati ya dakatari inayoonesha kwamba muombaji hana matatizo ya
kuona, kusikia wala hana maradhi ya kuambukiza kutoka Zahanati, kituo cha afya
au hospitali inayokubalika
9. Barua ya utambulisho kutoka katika taasisi ya Kiislamu
inayotambulika au masheikh (Wanawazuoni) wawili wanaokubalika kuelezea tabia na
maadili ya muombaji (Tazkiya)
10. Cheti cha kusilimu kwa wale ambao sio Waislamu wa kuzaliwa
MUDA WA KUWASILISHA MAOMBI TIF
Maombi yaliyokamilika na
yaliyokidhi mashati yote yaliyoelezwa hapi juu yaifikie Idara ya Da’wah ya TIF katika
ofisi za The Islamic Foundation kabla ya tarehe 21 Ramadhani, 1438 Hijriya sawa
na tarehe 16 Juni 2017 saa 12:00 jioni.
KWA MAWASILIANO ZAIDI:
Piga Namba za Simu Zifuatazo
0785 955 859 / 0715 955 859 /
0762 715 311 Katibu Mkuu TIF
Barua pepe: tifgsecretary@gmail.com
0784 364 969 Mkurugenzi Wa Da’wah
TIF
Barua pepe: kundyaismail@gmail.com
No comments:
Post a Comment