Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli akizungumza na wageni mbalimbali (hawaonekani pichani)
waliohudhuria katika Dhifa ya Kitaifa aliyomwandalia Rais wa Afrika Kusini
Jacob Zuma Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama
pamoja na mgeni wake Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma, Mama Janeth Magufuli
(Mke wa Rais), Mama Sizakele Zuma wakwanza kulia (Mke wa Rais wa Afrika Kusini)
wakati nyimbo ya Taifa ikipigwa katika Dhifa ya Kitaifa aliyomwandalia Rais wa
Afrika Kusini Jacob Zuma Ikulu jijini Dar es Salaam
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma akizungumza
katika Dhifa ya Kitaifa aliyoandaliwa na Mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam.
Viongozi mbalimbali wa Kisiasa na Serikali
wakiwa katika Dhifa ya Kitaifa aliyoandaliwa Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma
Ikulu jijini Dar es Salaam
Rais
wa Afrika Kusini Jacob Zuma akiwa amemshika mkono Waziri Mkuu Mstaafu Salim
Ahmed Salim wakati akizungumza jambo na Rais Msaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin
William Mkapa mara baada ya kumalizika kwa Dhifa ya Kitaifa Ikulu jijini Dar es
Salaam
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga makofi
pamoja na mgeni wake Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma wakati Bendi ya
Kilimanjaro “Wana njenje” ilipokuwa ikitumbuiza katika Ukumbi wa Ikulu katika
Dhifa ya Kitaifa aliyoandaliwa Rais Zuma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli akipiga makofi pamoja na mgeni wake Rais wa Afrika Kusini
Jacob Zuma wakati Bendi ya Kilimanjaro “Wana njenje” ilipokuwa ikitumbuiza
katika Ukumbi wa Ikulu katika Dhifa ya Kitaifa aliyoandaliwa Rais Zuma.
Rais
wa Afrika Kusini Jacob Zuma akisalimiana na Mwenyekiti wa Chama cha
ACT-Wazalendo Anna Mghwira mara baada ya Dhifa ya Kitaifa Ikulu jijini Dar es
Salaam, Pembeni ni Rais Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli akiagana na Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma mara baada ya
Dhifa ya Kitaifa aliyoandaliwa Rais huyo wa Afrika Kusini Ikulu jijini Dar es
Salaam.
Picha na Ikulu.
No comments:
Post a Comment