STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 20.05.2017
PONGEZI zimetolewa kwa Wafanyabiashara walioonesha
kitendo cha kizalendo na kishujaa kwa kuanza kutoa misaada kwa waathirika
waliopata maafa ya mvua zilizonyesha maeneo mbali mbali Unguja na Pemba pamoja
na upepo mkali uliotokea katika Mkoa wa Mjini Magharibi hivi karibuni na kuleta
athari kubwa.
Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein alitoa pongezi hizo
Ikulu mjini Zanzibar mbele ya viongozi wa Serikali, waandishi wa habari na Wafanyabiashara
walioongozwa na Mohammed Raza ambaye pia, ni Mwakilishi wa Jimbo la Uzini,
Ahmada Yahya Abdulwakil ambaye pia, ni Mwakilishi wa Kuteuliwa na Rais pamoja
na mfanyabiashara maarufu Said Nassor Popar.
Dk. Shein aliwapongeza
wafanyabiashara hao ambao pia, baadhi
yao ni viongozi kwa mwanzo mzuri walioanza kuuonesha kwa kufanya kitendo hicho
ambacho ni faraja kubwa kwa wananchi waliopata maafa pamoja na kutoa
ushirikiano mwema na Serikali yao.
Pia, Dk. Shein
hakuchelea kutumia fursa hiyo kutoa pongezi kwa vyombo vya habari kwa kutoa
taarifa ya maafa hayo sambamba na wito alioutoa kwa wale wote wenye uwezo
kuwasaidia wale waliokuwa hawana uwezo ambao wamekumbwa na maafa hayo.
Aidha, Dk. Shein
alieleza kuwa mvua hizo zimeweza kuleta athari kubwa hasa katika kisiwa cha
Pemba na kueleza kile alichokiona katika ziara yake hivi karibuni kisiwani humo
ambapo kabla ya hapo alifanya ziara kama hiyo katika maeneo ya Unguja hasa
katika Mkoa wa Mjini Magharibi ambao ulikumbwa na mafuriko yaliotokana na mvua pamoja na upepo mkali.
Dk. Shein alieleza kuwa
kutokana na juhudi zilizochukuliwa na Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi ,
Mawasiliano na Usafirishaji kwa hivi
sasa hakuna barabara wala daraja lisilopitika katika yale yalioharibika na mvua
hizo za masika katika barabara za Unguja na Pemba.
Alieleza kuwa matokeo
hayo yote ni shani ya Mwenyezi Mungu hivyo wananchi wanatakiwa wawe na subira
na uvuvilivu huku akiahidi kuwa Serikali itaendelea na juhudi za kuhakikisha wananachi
wanapatiwa misaada na maeneo yalioathirika na mvua yanafanyiwa utaratibu maalum
ili yasijekuleta madhara katika mvua
zijazo.
Dk. Shein alieleza kuwa
Serikali itaendelea kupokea misaada mengine itakayotolewa huku akitoa nasaha
zake kwa wafanya biashara hasa katika kuelekea Mwezi Mtukufu wa Ramadhani
kuacha kupandisha bei za bidhaa hasa vyakula kwani Serikali imeamua kwa
makusudi kusamehe sehemu ya ushuru wa bidhaa za vyakula ili wafanyabiashara
wawauzie wananchi bidhaa hizo kwa urahisi lakini kinachotokea ni tofauti.
Hivyo, Dk. Shein
alitumia fursa hiyo kuwataka baadhi ya wafanyabiashara kuacha mtindo huo mara
moya na kusisitiza kuwa iwapo wataendele nao serikali haitowavumilia na
kusisitiza kuwa Serikali ikiona hilo linaendelea itaurejesha ushuru huo wa
bidhaa za vyakuwa wakati wa mwezi wa Ramadhani kwani wananchi wamekuwa
hawafaidiki na chochote.
Dk. Shein
aliwahakikishia wananchi kuwa matarajio yake makubwa kuwa hapatakuwa na
ubabaishaji wala hadaa katika ugawaji wa misaada hiyo inayotolewa na
wafanyabiashara na ile itakayotolewa na Serikali kwani Kamisheni inayosimamia misdaa
hiyo ina wajumbe weledi.
Katika kupambana na
athari na maafa ya mvua aliahidi kuwa kwa upande wa Bwawa la Mwanakwerekwe
ambapo maji hutuama, kupitia Mradi wa Huduma za Jamii Mijini (ZUSP) Awamu ya
Pili, maji hayo yataondoshwa kwa kuelekwezwa pwani pamoja na kujenga daraja la
kisasa katika eneo la Kibondemzungu.
Alisema kuwa Serikali
inafanya tathmini juu ya athari zote zilizotokea katika maeneo mbali mbali ya
Unguja na Pemba pamoja na athari ya upepo mkali uliotokea katika maeneo ya Mkoa
wa Mjini Magharibi huku akisisitiza akuwa Serikali ni lazima itafute jitihada
za kujihami na kukushanya uwezo kwa ajili ya maafa.
Dk. Shein alisisitiza
kuwa ni vyema Serikali ikaangalia pale inapojenga barabara ni busara ikajengwa
na mitaro ya kupitishia maji kwani athari kubwa iliyotokea katika miundombinu
ya barabara nyingi hapa nchini imetokana na barabara kukosa mitaro.
Akitoa nasaha zake kwa
niaba ya wafanyabiashara hao Mohammed Raza alieleza kuwa wafanyabiashara wa
ndani na nje ya Zanzibar wataendelea kuwasaidia ndugu zao waliokumbwa na
mafuriko na athari za upepo ambapo misaada hiyo ikiwemo ya vyakula, fedha
taslim na vifaa vya ujenzi itasaidia hasa katika kipindi cha Mwezi wa Ramadhani
unaokaribia.
Raza alisema kuwa
kitendo hicho walichokifanya ni utamaduni wa Wazanzibari wa kusaidiana wakati
wa furaha na shida ambapo kwa upande wake ametoa fuso nne za vyakula vikiwemo
sukari pakiti 500, unga wa ngano pakiti 500, mafuta ya kupikia katuni 100.
Nae Ahmada Yahya
Abdulwakil alimkabidhi Rais TZS milioni 10 kwa Unguja na Pemba pamoja na
kuahidi msaada wa nondo tani mbili za milimita 10 zenye thamani ya TZS milioni 3
ambapo kwa upande wa mfanyabiashara Said
Nassor Popar ametoa idadi kama hiyo ya vyakula kupeleka kisiwani Pemba ambako vitagawiwa
kupitia Ofisi husika, pamoja na tende na sabuni.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment