Habari za Punde

Wafanyabiashara Wakabidhi Msaada wa Chakula Kwa Wananchi Waliuopata Maafa ya Upepo na Mvua za Masika.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati)akipokea fedha taslimu za Kitanzanuia Shilingi Millioni kumi kutoka kwa Mwakilishi wa kuteuliwa na Rais na Mfanyabishara Mhe,Ahmada Yahya Abdulwakil   katika hafla ya Msaada wa Chakula kwa waathirika na maafa ya Mvua za Masika na upepo mkali uliotokea hivi karibuni vilivyotolewa leo na Wafanyabiashara mbali mbali katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar,(wa pili kulia) Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Mhe,Mohamed Raza Daramsi
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia)akipokea msaada wa Chakula kutoka kwa Hassan Mohamed Raza kwa waathirika na maafa ya Mvua za Masika na upepo mkali uliotokea hivi karibuni,chakula hivyo vikiwemo Unga wa Ngano,Mafuta,Mchele na Sukari, vilivyotolewa leo na Wafanyabiashara mbali mbali katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar (wa pili kulia) Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Mhe,Mohamed Raza Daramsi na (kushoto) Mfanyabiashara Said Bophar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto)akizungumza na wafanyabishara katika hafla ya Msaada wa Chakula kwa waathirika na maafa ya Mvua za Masika na upepo mkali uliotokea hivi karibuni, vilivyotolewa na Wafanyabiashara mbali mbali katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar leo,(wa pili kulia) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe.Ayoub Mohamed Mahmoud
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akizungumza na wafanyabishara mbali mbakli katika hafla ya kukabidhi Msaada wa Chakula kwa waathirika na maafa ya Mvua za Masika na upepo mkali uliotokea hivi karibuni,mazungumzo hayo yalifanyika leo  katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar
Baadhi ya Waandishi wa habari na Viongozi mbali mbali waliohudhuria katika hafla ya kukabidhi ya Msaada wa Chakula kwa waathirika na maafa ya Mvua za Masika na upepo mkali uliotokea hivi karibuni, vilivyotolewa leo na Wafanyabiashara mbali mbali katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) ,[Picha na Ikulu.] 20/05/2017.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.