STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar
25.08.2017
MAKAMO Mwenyekiti wa CCM Zanzibar
na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein,
ameweka jiwe la Msingi katika Tawi la CCM Tibirinzi na kusisitiza kuwa siasa
sio ugomvi.
Dk. Shein
aliyasema hayo mara baada ya kuweka jiwe la Msingi la Tawi hilo la Tibirinzi
ambalo lilitiwa moto mnamo mwaka 2015 na watu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa
chama kimoja wapo cha upinzani hapa Zanzibar.
Makamo Mwenyekiti huyo wa CCM
Zanzibar, alieleza kuwa siasa ya vyama vingi wameitaka wenyewe wananchi hivyo
jambo la kushangaza kuwa baadhi ya wanasiasa wamelichukulia jambo hilo kuwa ndio
njia moja wapo ya kujengeana chuki, kutukanana na kutovumiliana.
Aliongeza kuwa kwa vile chama cha
CCM ndio fundi wa siasa tokea ASP na TANU kitaendelea kuvisomesha vyama
vyengine vya siasa nini maana ya siasa na chama cha siasa kinatakiwa kiwe vipi
katika suala zima lakuvumiliana, kutojengeana chuki.
Dk Shein alisema kuwa si vyema
siasa ikawagawa watu na kuwafanya wakaishi kwa uadui na badala yake watu
wanatakiwa kuishi kwa kushirikiana, kupendana na kustahamiliana kwani siasa ni
uvumilivu na sio ugomvi.
“Mimi nawaambia
wana CCM wenzangu, mfanye kazi za chama vizuri bila woga na muhakikishe mnafanya
vikao vya mara kwa mara katika Tawi letu hili, ili muweze kuleta maendeleo
katika chama chetu”alisema Dk. Shein.
Aidha, Dk. Shein alisema kuwa Chama
cha Mapinduzi (CCM) kitaendelea kustahamili na kuwa na subira lakini ifike
wakati na vyama vyengine vitambue kuwa subira nayo huwa na mipaka kwani lengo
la chama ni kuwapelekea maendeleo wananchi.
Alieleza kuwa kitendo cha kulichoma
moto Tawi hilo la CCM kimeonesha wazi kuwa baadhi ya vyama vya siasa bado ni
wanagenzi wa siasa na dhana yao kuwa siasa ni chuki, ugomvi na uhasama hali inayoonesha
kuwa bado hawajaujua umuhimu na malengo ya kuwepo kwa vyama vingi.
Hivyo, Makamo Mwenyekiti wa CCM
Zanzibar alisisitiza kuwa tukio hilo la kuchomewa Tawi lao huilo la CCM liwe la
mwisho huko akisisitiza kuwa CCM inafuata miongozo ya dini ikiwa ni pamoja na
kukubali suluhu na kutambua kuwa pande mbili zikifarakana ni vyema zikakaa
pamoja na kushauriana sambamba na kuwa na subira na kuvumiliana.
Sambamba na hayo, Dk. Shein ambaye
ndio alilolijenga Tawi hilo baada ya kutiwa moto na mnamo tarehe 31 Mwezi Mei
mwaka huu alifika Tawini hapo kwa ajili ya kulikagua na kujionea hujuma
zilizofanywa za kutiwa moto tawi hilo.
Katika kuhakikisha Tawi hilo
linakuwa la kisasa na wanachama wake wanaendelea na shughuli zao za chama,
aliwataka viongozi wa CCM Mkoa huo wakiwemo Wawakilishi pamoja na Mbunge wa
Viti Maalum kulimalizia kwa kuliweka milango, shata za madirisha na umeme.
Nae Naibu Katibu Mkuu wa CCM
Zanzibar Abdalla Juma Mabodi alitoapongezi zake kwa Rais Dk. Shein kwa juhudi
zake hizo za kulijenga upya tawi hilo na kuwa la kisasa huku akiahidi kuwa
Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui itatoa msaada wa viti kwa ajili ya Tawi hilo.
Mapema wanachama wa CCM wa tawi
hilo walitoa pongezi za pekee kwa Dk. Shein kwa kulijenga upya tawi lao hilo
baada ya kuchomwa moto na kuteketezwa mnamo Machi 10 mwaka 2016 na kupelekea
uharibifu mkubwa.
Mapema Dk. Shein alifika Kiziwani
Shungi na kuzindua uchumaji wa karafuu katika Wilaya ya Chake Chake ambapo
alishiriki kikamilifu katika uchumaji wa zao hilo katika shamba la mikarafuu la Bi Fatma Hamad Said
ambalo kwa hivi sasa linashughulikiwa na Muhene Ali Salum lenye ukubwa wa eka
4.2 na mikarafuu 197.
Mkuu wa Idara
ya Misitu na Mali zisizorejesheka Pemba, Saidi Juma alisema Wilaya ya Chake
Chake imeshakodisha mashamba 85 yenye thamani ya TZS milioni 298.3.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment