Habari za Punde

Usajili wa Dirisha Dogo Kufungwa Kesho Alhamisi.Hakuna Kuongeza Muda -Katibu ZFA.

Na: Abubakar Khatib Kisandu, Zanzibar.
Dirisha la uhamisho na usajili rasmi linafungwa kesho Alhamis Agost 17 majira ya saa 6:00 za usiku ambapo Makocha na Viongozi wengine wa Vilabu wamezidi kuwa bize kutafuta wachezaji wanaowahitaji ili kuziboresha timu zao katika msimu mpya wa mwaka 2017-2018.

Akizungumza na Mtandao huu katibu mkuu wa ZFA Mohd Ali Hilali “Tedy” amesema usajili unafungwa kesho Agost 17 na wao ZFA hawatoongeza siku wala muda ukifika wakati uliopangwa zoezi hilo litapigwa kufuli.

“Ni kweli zoezi la uhamisho na usajili linafungwa kesho Alhamis saa 6:00 za usiku na wala hatutarajii kuongeza siku wala saa, muda ukifika zoezi hilo litafungiwa”. Alisema Tedy.

Chama cha Soka Visiwani Zanzibar “ZFA” kilitangaza zoezi la uhamisho na usajili kwa msimu wa mwaka 2017-2018 kufunguliwa July 17, 2017 na kumaliza kesho Agost 17, 2017.

Zoezi hilo ni kwaajili ya Maraja yote kuanzia ligi kuu soka ya Zanzibar, ligi daraja la kwanza Taifa, la Pili Taifa hadi ligi za Madara ya Wilaya.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.