Na Shaibu
Kifaya----Mkoani.
Jamii
imeshauriwa kujitokeza kwa wingi katika kujiunga na vikundi vya ushirika ili kuweza kujikwamua na umasikini na
kuondokana na hali duni ya utegemezi wa kiuchumi na kuweza kujiletea maendeleo
katika familia zao.
Hayo
yalielezwa na mshikafedha
wa kikundi cha ufugaji nyuki cha TUSHIKAMANE
, Moh’d Khamis Amani, kilichopo katika kijiji cha Likokuu Shehia ya Chokocho
Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba, wakati alipokua akizungumza na mwandishi
wa habari hizi.
Alisema kuwepo kwa vikundi kama hivi kutatoa muamko mkubwa kwa vijana ambao bado hawajataka
kujishuhulisha na kazi yoyote hivyo kujikusanya pamoja kutawasaidia kujiendeleza katika shuli zao mbali mbali
za kimaisha na kuweza kujipatia kipato
cha halali.
Akizungumzia
changamoto wanazozipata Mwenyekiti wa
kikundi hicho Omari Hamadi Abdala ,alisema
jambo kubwa linalowarejesha nyuma ni
kuweka mizinga yao kwa muda mrefu bila
ya kupata mafanikio yoyote .
Aliongeza
kuwa bado hawajapata soko la uhakika la kuuzia asali na kulazimika kutafuta
soko katika Wilaya ya Chake Chake, ambako nako bado hakujawa na uhakika wa kuuza
kwa bei yenye kuleta tija.
“
Tunaiomba Serikali kuharakisha kuwapatia soko hilo kama ilivyo katika mipango
yao, ili tuweze kupambana na Umaskini unaotukabili “ alisema Mwenyekiti huyo.
Na
kwa upande wake, Said Makame Ayubu, ambae ni miongoni mwa wana
kijiji cha Likokuu shehia ya chokocho ,alisema kuwepo kwa
kikundi kama hichi cha ufugaji nyuki kunatoa muamko mkubwa kwa vijana ambao
bado hawajataka kujishuhulisha na kazi yoyote.
Kikundi
hicho cha ufugaji nyuki cha TUSHIKAMANE kilianzishwa
mwaka 2005 kikiwa na wanachama sita wakiwa
ni wanawake wawili na wanaume wane na walikuwa wakitumia zana zao za asili za
kutegea Nyuki hao.
No comments:
Post a Comment