Habari za Punde

HATIMAYE WANANCHI WANAOTAKIWA KUPISHA MRADI WA SHANTA GOLD MINE WILAYANI IKUNGI WATEKELEZEWA MALIPO YAO

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliowahusisha wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi, Sambaru na Mulumbi kwa ajili ya kulipa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Ltd.
Wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi, Sambaru na Mulumbi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumza katika mkutano wa hadhara kwa ajili ya kulipwa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Ltd.
Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mining Ltd Philbert Rweyemamu akielezea utaratibu wa ulipaji fidia kwa wanufaika.
Wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi, Sambaru na Mulumbi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumza katika mkutano wa hadhara kwa ajili ya kulipwa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Ltd.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisalimiana na Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mining Ltd Philbert Rweyemamu mara baada ya mkutano wa hadhara kwa ajili ya kulipwa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa uchimbaji madini.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisalimiana na wananchi mara baada ya mkutano wa hadhara kwa ajili ya kulipwa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa uchimbaji madini.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliowahusisha wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi, Sambaru na Mulumbi kwa ajili ya kulipa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Ltd.
Wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi, Sambaru na Mulumbi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu Akizungumza katika mkutano wa hadhara kwa ajili ya kulipwa fidia za wanufaika kwa ajili ya kupisha Mradi wa Kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Ltd. 



Na Mathias Canal, Singida
Kampuni ya Uchimbaji wa Madini ya dhahabu (Shanta Gold Mining Limited) iliyopo katika kijiji cha Sambaru Kata ya Mang’onyi Wilayani Ikungi, Mkoani Singida huenda ikaanza uchimbaji wa madini ya dhahabu hivi karibuni baada ya kuanza kulipa fidia ya zaidi ya Bilioni 1.6 wanufaika wa awamu ya pili inayohusisha wananchi kutoka Vijiji vitatu vya Mang'onyi, Sambaru na Mulumbi.


Kampuni hiyo tayari imekamilisha ulipaji wa awamu ya kwanza kwa kulipa zaidi ya Milioni 900.2 Wanufaika waliolipwa fedha hizo wanaotokana na mazoezi mawili ya uthamini yaliyofanywa kwenye eneo la mradi kwa ajili ya upanuzi wa kambi.


Malipo hayo yatakamilisha umiliki wa maeneo hayo kwa Kampuni ya Shanta Gold mining kwa ajili ya uchimbaji na kuwafanya wananchi hao kupisha mradi wa uchimbaji dhahabu pasina kinyongo chochote.


Malipo hayo ya awamu ya pili na ile ya kwanza yamelipwa kwa wanufaika wote wa fidia katika Vijiji vyote vilivyopo Katika Kata ya Mang'onyi yanaondoa malalamiko ya muda mrefu ya wananchi wa maeneo mbalimbali waliopo kwenye eneo la mradi huo waliotaka kufahamu hatima ya malipo yao.


Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliowahusisha wananchi wa Kijiji cha Mang’onyi na wawakilishi wa kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Gold Mining Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe Miraji Jumanne Mtaturu alisema kuwa kampuni hiyo inapaswa kutumia muda mfupi katika ulipaji wa fidia kama ilivyofanya katika awamu ya kwanza.


Alisema kuwa Kampuni hiyo ya uchimbaji imeanza kutekeleza sheria ya madini inayoelekeza miezi sita kabla ya kuanza uchimbaji wawekezaji wanapaswa kuanza kulipa fidia.


Naye Meneja wa Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Shanta Gold Mining Ltd Philbert Rweyemamu alisema kuwa kampuni yake imeanza kutekeleza maelekezo yaliyotolewa na Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu mwezi Disemba 2016 ya kuwalipa wanufaika hao fidia ambayo ni hatua muhimu ya utekelezaji wa mradi huo.


Alisema kuwa malipo yanafanywa na kampuni hiyo chini ya usimamizi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya sambamba na wenyeviti wa serikali za vijiji vyote vilivyopo ndani ya mradi.


Kuanza kwa uchimbaji wa madini katika eneo hilo kutaibua ajira nyingi kwa wananchi Wilayani Ikungi na Taifa kwa ujumla jambo litakalosaidia ukuzaji wa pato la mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla wake.


Katika Awamu ya Kwanza Kampuni ya Shanta Gold Mining Ltd iliwalipa wanufaika 92 wenye umiliki wa Viwanja 121 thamani yake ikiwa ni Shilingi 902,412,247.00 Hulu awamu hii ya Pili wakilipwa Wamiliki 114 wenye Viwanja 156 vyenye thamani ya Shilingi 1,663,112,018.01


Aidha, Kuanzia leo Septemba, 2017 wanufaika wa fidia wameanza kufanya uhakiki wa malipo yao na ufunguaji Akaunti kwa ajili ya malipo ikiwa ni matakwa ya kisheria.


Akizungumza kwa niaba ya wananchi, Mwenyekiti wa Kijiji Cha Mang'onyi Ndg Mohamed H. Ramadhani alimshukuru Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu kwa kutoa maagizo ya kulipwa haraka fidia za kila wanufaika Jambo ambalo limetekelezeka kwa haraka katika kipindi Cha muda mfupi.


Sambamba na hayo aliongeza kuwa Mkuu huyo wa Wilaya anafanya kazi kubwa katika kuwaunganisha wananchi wote ili kupata stahiki zao na kufurahia Rasilimali za Nchi yao.


MWISHO

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.