Habari za Punde

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Azungumza na Mchungaji Joseph. Ofisini Kwake Vuga.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na Mkuu wa Makanisa ya EFATHA Duniani k Akizungumza na Mkuu wa Makanisa ya EFATHA Duniani Mchungaji Joseph E.Mwingira, alipofika Ofisini kwake kwa mazungumzo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimkabidhi zawadi ya mlango wa Zanzibar (Zanzibar Door) mchungaji Joseph E. Mwingira. baada ya mazungumzo yao. yaliofanyika Ofisi ya Makamu Vuga Zanzibar.(Picha na OMPR)

Na. Mohammed Muombwa OMPR.
Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema Tanzania itaendelea kuilinda historia yake ya kudumisha mashirikiano na maelewano ya waumini wa dini mbali mbali nchini.

Makamo wa Pili wa Rais ameyasema hayo leo afisini kwake Vuga wakati alipokuwa akizungumza na Mkuu wa makanisa ya EFATHA duniani mchungaji Joseph E. Mwingira.

Amesema msingi wa amani ya Tanzania unatokana na mashirikiano ya karibu kati ya viongozi wa kisiasa na dini ambao wote kwa pamoja wanahubiri kwa wafuasi wao suala zima la kudumisha amani na utulivu.

Amesema Zanzibar tangu zamani wananchi wake wamezowea kuishi na watu wa dini mbali mbali kwa amani, utamaduni ambao hauna budi kuimarishwa kwani bila ya amani hakuna maendeleo.

Mkuu wa Makanisa mchungaji Joseph E. Mwingira kwa upande wake amefurahishwa na uhusiano uliokuwepo Zanzibar kati ya waumini wa dini mbali mbali na akasisitiza kudumishwa kwa uhusiano huo kwa maslahi mapana ya nchi.

Amesema ni vyema kwa Serikali kuwachukulia hatua watu wote wanaotaka kuvuruga amani kwani amani ikishatoweka ni vigumu kuirejeshwa.

Mchungaji huyo amesema Zanzibar ina sifa nyingi nzuri nje, sifa ambazo amesisitiza ni vyema zikadumishwa kwa maslahi ya uchumi wa nchi.

Kiongozi huyo wa dini ameyataja mambo manne ambayo amewataka viongozi waliopo madakarakani kuyazingania. Mambo hayo ni pamoja na kutambua nafasi ya Mungu, viongozi kutambua kuwa wanatumikia watu, kuhimiza amani na maendeleo na kuwapenda watu.

Amesema mambo hayo manne yakifuatwa Tanzania itajipatia maendeleo ya haraka kwa kipindi kifupi.


Wakati huo huo Mkuu huyo wa Makanisa ameahidi kichangia viafaa vya thamani ya milioni kumi (Tshs. 10,000,000) kwa hospitali ya Mnazi ili kuongezea nguvu Serikali kuimarisha huduma za afya kwa jamii.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.