Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPC, Deo Kwiyukwa, akizungumza katika mkutano huo na kisha kumkaribisha Mwenyekiti wa Bodi ya TPC, Dk. Harun Kondo (katikati), kuzungumza na Menejimenti na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi wa shirika hilo, jijini Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa Bodi ya TPC, Dk. Harun Kondo (katikati), akizungumza na Menejimenti na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi wa TPC, jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPC, Deo Kwiyukwa na kulia ni Kaimu Katibu wa Shirika, Zuhuru Pinde.
Mwenyekiti wa Bodi ya TPC, Dk. Harun Kondo (wa pili kulia), kuzungumza na Menejimenti na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi wa TPC, jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPC, Deo Kwiyukwa na kulia ni Kaimu Katibu wa Shirika, Zuhuru Pinde.
Baadhi ya viongozi wa Vyama vya wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakiandika maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya TPC, Dk. Harun Kondo, wakati akizungumza nao pamoja na Menejimenti ya TPC, jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya viongozi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC) na wa Vyama vya wafanyakazi wa shirika hilo, wakisikiliza maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Mwenyekiti wa Bodi, Dk. Harun Kondo, katika mkutano wao huo, Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa Bodi ya TPC, Dk. Harun Kondo, akifafanua jambo wakati wa akizungumza na Menejimenti na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi wa TPC, Dar es Salaam leo. Kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPC, Deo Kwiyukwa.
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari, wakichukua habari wakati Mwenyekiti wa Bodi ya TPC, Dk. Harun Kondo, alipokuwa akizungumza katika mkutano huo.
Baadhi ya viongozi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC) na wa Vyama vya wafanyakazi wa shirika hilo, wakisikiliza kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Mwenyekiti wa Bodi, Dk. Harun Kondo, katika mkutano wao huo.
Baadhi ya viongozi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC) na wa Vyama vya wafanyakazi wa shirika hilo, wakifuatilia kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Mwenyekiti wa Bodi, Dk. Harun Kondo, katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa Bodi ya TPC, Dk. Harun Kondo (kushoto), akifafanua jambo wakati akizungumza na Menejimenti na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi wa TPC, jijini leo. Kushoto ni Meneja Mkuu Uendeshaji wa shughuli za shirika, Hassan Mwang'ombe na wa pili ni Meneja Mkuu wa TPC, Macrice Mbodo.
Baadhi ya viongozi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC) na wa Vyama vya wafanyakazi wa shirika hilo, wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Mwenyekiti wa Bodi, Dk. Harun Kondo, katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa Bodi, Dk. Harun Kondo, akifafanua jambo katika mkutano huo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Elia Madulesi (kulia), akiteta jambo na Ofisa Uhusiano wa shirika, Joseph Ngowi.
Baadhi ya viongozi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC) na wa Vyama vya wafanyakazi wa shirika hilo, wakisikiliza maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Ofisa Mtendaji Mkuu, Deo Kwiyukwa katika mkutano huo, leo Dar es Salaam.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPC, Deo Kwiyukwa, akijibu baadhi ya maswali ya waandishi wa habari, wakati wa mkutano huo.
Mwenyekiti wa Bodi ya TPC, Dk. Harun Kondo (katikati), akizungumza na Menejimenti na Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi wa TPC, jijini Dar es Salaam leo.
MAELEZO YA MWENYEKITI WA BODI WAKATI WA KIKAO NA MENEJIMENTI NA
VIONGOZI WA VYAMA VYA WAFANYAKAZI TAREHE 14 SEPTEMBA 2017
NDUGU POSTAMASTA MKUU
MENEJIMENTI YA SHIRIKA LA POSTA
NDUGU VIONGOZI WA VYAMA VYA WAFANYAKAZI
·
Kwanza kabisa napenda
kuchukua fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema, kwa kutuwezesha
kujumuika hapa na kushiriki pamoja katika kikao hiki.
·
Pia napenda niwakaribishe
na niwashukuru wote mliofanikiwa kufika katika kikao hiki.
Kama mtakumbuka
ni takriban miezi sita tangu tulipokutana tena hapa ikiwa ni kikao changu cha
kwanza kabisa kukutana na nyie viongozi wa vyama vya wafanyakazi
Ari
mliyonionyesha wakati wa kikao hicho ndiyo imenisukuma kutaka tena leo hii
kuzungumza na nyie ikiwa ni kama mwaka mmoja tangu Bodi yetu ilipoteuliwa.
Kikao cha
wakati ule kilikuwa ni pamoja na kukumbushana juu ya wajibu wa Bodi na
Menejimenti ya shirika la posta , na pia ililenga kujitambiulisha na
kufahamiana
Ndugu viongozi wa
wafanyakazi
Kama mnavyojua shirika letuliko kwenye kipindi cha
mabadiliko,
·
Napenda niwaeleze wazi kabisa kuwa mimi
binafsi na Bodi ya Wakurugenzi tunayo dhamira ya dhati ya kuhakikisha
Menejimenti na Wafanyakazi wote wa Shirika ambao ni zaidi ya 1000 mnashiriki na
kuchangia mabadiliko ya kiutendaji ndani ya Shirika hili.
·
Kupitia Wizara yetu mama ya Ujenzi, Uchukuzi
na Mawasiliano nao wanadhamira hiyo.
·
Baadhi yetu tumeshuhudia dhamira hiyo njema
wakati Mheshimiwa Waziri Prof. Makame M. Mbarawa na aliyekuwa Naibu Waziri wake Edwin A. Ngonyani walipokutana na
Menejimenti na Wafanyakazi na pia kutembelea baadhi ya sehemu za kazi katika
Posta yetu Kuu ya Dar es Salaam yaani GPO.
·
Kwa bahati nzuri hii ndio dhamira ya
Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dr. John Pombe Joseph Magufuli ya
kuhakikisha Taasisi na Mashirika yake ikiwa na pamoja na Shirika la Posta
yanashiriki na kuchangia jitihada za kuleta maendeleo ya haraka.
·
Napenda Shirika letu hili lisiwe kikwazo
bali kichocheo cha kufanikisha jitihada hizi. Tusiwaangushe Watanzania.
Ndugu viongozi wa
wafanyakazi
> Mimi
binafsi nimekuwa nakutana na viongozi wa Wizara mara kwa mara kuzungumza juu ya
changamoto mbalimbali ambazo shirika linakabiliana nazo ili kupata ufumbuzi
wake ,Wizara imekuwa ikinipa ushirikiano mkubwa.
Pia nimekuwa na vikao vya mara kwa mara na Wizara ya
Fedha kupitia kwa Msajili wa Hazina kutatua baadhi ya changamoto zinazolikabili
Shirika zikiwemo madeni na kodi mbalimbali ambazo tunadaiwa.
Bila shaka mtakuwa mna taarifa kuwa baadhi ya madeni
ya pensheni za wastaafu wa Jumuia ya Afrika Mashariki tuliyokuwa tunaidai
Serikali tumeshaanza kurejeshewa.
1. CHANGAMOTO ZA
SHIRIKA
Kama
mnavyofahamu mbali na changamoto za mtaji pia shirika linakabiliwa na
changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na ;
Ø Mapungufu
katika kusimamia nidhamu, uadilifu, weledi na upimo wa utendaji, kubadilisha
mitizamo ya Wafanyakazi, udhibiti wa mapato na matumizi ya Shirika.
Ø Kurekebisha
maslahi ya Wafanyakazi na kuwaendeleza ili kumudu kazi katika mabadiliko ya
teknolojia.
Ø Kuboresha
miundombinu ya Shirika la Posta ikiwa ni pamoja na miliki.
Ø Kulifanya
Shirika kuwa Taasisi shirikishi katika kutekeleza na kufikia malengo ya kitaifa
na kimataifa.
Ø Kuongeza
ufanisi wa kiutendaji ili kukuza wingi na ubora wa biashara pamoja na kuhakikisha
kunakuwepo faida kwa Shirika na kutoa gawio kwa Serikali.
Ø Kupanua
mtandao na wigo wa soko ili wananchi wote hadi huko vijijini wapate kufikiwa na
huduma bora na za kisasa.
Ili kufanikisha
azma hiyo ,Bodi imechukuwa hatua mbali mbali ikiwa ni pamoja na kusimamisha
,kuachisha na kufukuza wale wote wanaoonekana ni kikwazo cha juhudi hizo.
2. FURSA ZA
SHIRIKA
Ndugu viongozi
wa wafanyakazi,
Pamoja na
changamoto zilizopo, lakini tunazo fursa nyingi tu za kupanua na kuboresha
biashara zetu. Mheshimiwa Waziri alisisitiza sana juu ya jambo hili:-
·
Miliki za Shirika ikiwa ni pamoja na majengo
na viwanja vilivyoko kwenye “prime areas” za miji mbalimbali
hapa nchini. Ingawa hili lina changamoto ikiwa ni pamoja na ukosefu wa
rasilimali fedha,kuendelea kwa shirika kuwa chini ya uangalizi, lakini kwa
kiwango kikubwa ni fursa nzuri na yote haya yanafanyiwa kazi na serikali yetu.
·
Mtandao wetu mpana wa kitaifa wa ofisi
zipatazo 400 zilizounganishwa na ofisi 660,000 duniani unawezesha kupanua na
kuboresha zaidi biashara zetu ndani na nje kwa minajili ya kukuza mapato.
·
Matumizi mazuri ya TEHAMA yanawezesha
kuanzisha biashara mpya za kimtandao kama Hybrid mail, Digital Stamps, na
huduma jumuishi mahali pamoja (Unified Community Services) au huduma Express.
·
Ushindani licha ya kuwa ni changamoto lakini
kwa upande mwingine ni fursa nzuri tu ya kuboresha, kupanua na kubuni huduma
mpya.
3. MALENGO YA SHIRIKA
Ndugu viongozi
wa wafanyakazi,
·
Napenda kuchukua fursa hii kuwakumbusha
wajibu wetu wa uwajibikaji kwa watumishi wa kada
zote ndani ya Shirika kwa kujenga nidhamu ya kazi, kujituma, kuheshimu kanuni
na taratibu, kuongeza ubunifu na kufanya kazi kwa ufanisi wenye tija. Lazima
tubadilishe mitazamo (mind sets) yetu ili tuondokane na kuendesha shughuli kwa
mazoea yaani “business as usual”.
·
Natambua kuwa maslahi ya viongozi na ya
wafanyakazi siyo ya kiwango cha kuridhisha lakini lazima mzingatie kuwa maslahi
bora kwa watumishi yanatokana na ongezeko la ufanisi na tija.
4. MAFANIKIO YA BODI.
Napenda kuwajulisha kuwa katika kipindi hiki kifupi kwa ushirikiano mzuri
uliokuweko kati ya Bodi na menejimenti
kunekuwa na mengi kama yafuatavyo;
(a)Kuanzishwa kwa kampuni tanzu 4
Bodi imeridhia kuanzishwa kwa kampuni tanzu mpya nne ambazo
zimekwishasajiliwa kisheria.kampuni hizo ni;
i.
Posta Logistics Ltd,
ii.
Posta Freight and Forward,
iii.
Posta Microfinance,
iv.
Posta Digital.
Kampuni hizo zitakapoanza kufanya kazi zitakuwa kichocheo cha kuliingizia
mapato shirika na hivyo kuwezesha kuboresha maslahi ya wafanyakazi na kuboresha
zaidi mazingira ya kazi.
(b)Kuridhia muundo mpya wa shirika
Bodi imeridhia mapendekezo ya muundo mpya yaliyowasilishwa na
menejimenti. Muundo huo umewasilishwa kwenye mamlaka ya juu ili uweze kuridhiwa
na kuanza kutumika mapema iwezekanavyo.
Lengo la muundo huo ni kuboresha utendaji , kuondoa urasimu na kuboresha
maslahi ya wafanyakazi.
(C) Miliki za
shirika
kwa kipindi cha mwaka mmoja tangu bodi iteuliwe kwa kushirikiana na
menejimenti na watendaji wake shirika limeweza kuweka kumbukumbu sahihi za viwanja/ miliki za shirika zipatazo
198,ambazo kati ya hizo hati 154 zimekwishapatikana na nyingine zinafuatiliwa kwa karibu .
(d)Ukusanyaji madeni
Bodi ilipoanza kazi yake rasmi
mwishoni mwa mwaka jana ilikuta shirika linadai madeni ya zaidi ya
shilingi bilioni ‘10’.bodi kwa kushirikiana na menejimenti ya shirika iliweka
mkakati wa pamoja ambao uliwezesha kukusanya madenini ya shilingi bilioni 7.5
kwa kuwatumia wafanyakazi wa ndani.
(e) Jitihada za kubana matumizi
·
Shirika lilipitia upya
mikataba ya upangaji na kuirekebisha na kuhakikisha kuwa kila mpangaji ana
mkataba sahihi na pia matumizi yasiyo na tija yameendelea kupunguzwa.
·
Pia bodi ilipitia zabuni
mbalimbali na kubaini zabuni zilizokuwa na dosari na kuzirekebisha moja wapo
ikiwa ni ile ya valuation ambayo ilikuwa shilingi milion 245 na kuweza
kupunguza hadi milion 160.
·
Pia shirika lilifanikiwa
kutengeneza muundo mpya kwa kutumia wataalamu wake wa ndani na kuweza kuokoa shilingi milioni 700
zilizokusudiwa kutumiwa kwa ajili hiyo kwa kutumia wataalam kutoka nje.
(f) Kurejeshewa madeni ya pensheni
Baada ya juhudi za Bodi na Menejimenti kufanyika Serikali imeridhia
kurudisha madeni tuliyokuwa tunaidai Serikali ya shilingi bilion 3.9 ambayo ni
deni la pensheni za wastaafu wa lililokuwa Shirika la Posta na Simu la Afrika
Mashariki.
Mazungumzo kati ya Shirika la Posta na Serikali yamewezesha kufikia
makubaliano ambapo kwa sasa pensheni hizo zitakuwa zinalipwa na Serikali moja
kwa moja kwa wahusika .
(g)Payment switch
Mikakati mingine iliyofanywa na bodi na menejimenti mpya kwa katika
kipindi hicho ililenga katika kuboresha huduma au biashara zetu kwa mfano sasa
hivi mazungumzo yanaendelea kati yetu na TTCL kwa udhamini wa Wizara ya Fedha
ili kuona uwezekano wa kutumia payment switch ya TTCL .matumizi ya payment
switch hiyo yataenda sambamba na
uanzishwaji wa kampuni tanzu mpya nilizozitaja.
Na kama mnavyojua tumeanzisha mfumo mpya wa kutoa huduma kwa pamoja yaani
one stop shoping center ,mfumo ambao utawezesha huduma mbalimbali kupatikana
mahali pamoja.Mradi huo umeanza Posta Mpya na unaendelea kuboreshwa.
(h)Mikataba ya kibiashara.
Mikakati mingine mipya ambayo Bodi na Menejimenti imefanya ni kuingia
mikataba mipya na taasisi mbali mbali.
Kwa mfano hivi karibuni tumeingia mkataba na ATCL ambapo kampuni hiyo ya
ndege itatumia majengo yetu kwa ajili ya kutolea huduma zake na Shirika la
Posta litatumia ndege hizo kusafirishaji wa mifuko yake ya barua/vifurushi.
Shirika la Posta liko kwenye mazungumzo na taasisi mbalimbali kwa lengo
la kuutumia kikamilifu mtandao wa Posta kwa ajili ya kutoa huduma
mbalimbali,ikizingatiwa kuwa Posta iko kila Mkoa kila Wilaya na baadhi ya
Tarafa na Vijiji.
(i) Mapitio ya
kanuni na sheria za kazi
Shirika linapitia na kuandaa sheria na kanuni mpya za kazi ili ziweze
kuendana na maabadiliko ambayo yamekusudiwa ili kujenga mazingira ya kazi
yanayofaa kwa wakati wa sasa.
(i)Muonekano mpya wa Shirika
Kwa sasa shirika liko kwenye hatua
za mwisho za kuboresha muonekano
wa ofisi zake ikiwa ni pamoja na
kutambulisha nembo mpya ya Shirika. Lengo lake ikiwa ni kujipanga upya na kuja
kivingine.
Pia Shirika kwa kutumia wataalamu wake wa ndani limefanikiwa kuunda
mifumo mbalimbali ya TEHAMA.
5. MAWASILIANO
YA NDANI.
Nia ya kuwaiteni viongozi wa wafanyakazi ni
kuwajulisha yale yanayofanywa na viongozi wenu ili mtakapokutana na wafanyakazi
wenzenu muweze kuwajulisha yale yanayofanywa na viongozi wenu kwa niaba yao.
Natambua umuhimu wa mawasiliano katika taasisi yoyote ile, na jinsi
yanavyoweza kujenga daraja kati ya Bodi Menejimenti na wafanyakazi wa chini,
ndio maana nasisitiza vikao na mikutano ya mara kwa mara ifanyike ili kupeana
mrejesho na kupeana taarifa mbalimbali kwa lengo la kujenga umoja na
mshikamano.
·
Mawasiliano mazuri husaidia katika kukuza
maendeleo ya Shirika kwa ujumla. Kwa wafanyakazi
mawasiliano yatakuza utendaji wao wa kazi kwa sababu kutakuwa na uwazi juu ya
yanayoendelea na yatarajiwayo kutokea kwa maendeleo ya Shirika.
·
Vilevile kuwepo kwa mawasiliano mazuri
katika Shirika kutaongeza nguvu kazi na uwezo wa wafanyakazi katika ngazi zote
za Shirika kufanya kazi kwa pamoja kupunguza migogoro
na kufikia malengo ya Shirika.
Mawasiliano
ya wazi na ya mara kwa mara kati ya Bodi Menejimenti na wafanyakazi yataondoa
au kupunguza minongono na taarifa potofu
Ndugu viongozi
wa wafanyakazi.
·
Baada ya kusema haya ninapenda niwashukuru
tena kwa kuhudhuria kikao hiki nina imani tutaongeza bidii, tutashirikiana
vyema na kwa uwazi kwa lengo la kuleta mabadiliko chanya katika Shirika letu.
·
Mwisho nakaribisha maoni, maswali au
ufafanuzi mnaohitaji kwa ajili ya ustawi wa Shirika letu.
Asanteni kwa kuniskiliza.
No comments:
Post a Comment