STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 09.10.2017
RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein amemtumia
salamu za pongezi Rais wa Jamhuri ya Watu wa Uganda, Yoweri Kaguta Museveni kwa
kutimiza miaka 55 tokea kupata Uhuru kwa Taifa hilo.
Salamu hizo zilieleza kuwa
wananchi wa Zanzibar wanaungana na ndugu zao wa Jamhuri ya Watu wa Uganda
katika kusherehekea siku hii adhimu kwa
Taifa hilo.
Aidha, katika salamu hizo,
Dk. Shein alimuhakikishia Rais Museveni kuwa Zanzibar itaendeleza uhusiano na
ushirikiano mkubwa uliopo kati yake na Jamhuri ya Watu wa Uganda sambamba na
kuimarisha udugu uliopo kati ya wananchi wa Jamhuri ya Watu wa Uganda na
wananchi wa Zanzibar.
Sambamba na hayo, Rais Dk.
Shein alisisitiza juu ya haja ya kufanya kazi kwa pamoja katika kuimarisha
mashirikiano katika masuala mbali mbali yanayohusu Jumuiya ya Afrika Mashariki,
Umoja wa Afrika pamoja na masuala mbali mbali ya kimataifa.
Pamoja na hayo, Dk. Shein alitumia
nafasi hiyo kumtakia uongozi mwema Rais Museveni pamoja na kumtakia uonghozi
mwema wa Taifa hilo kwa amani na utulivu kwa maendeleo endelevu ya wananchi wa
Jamhuri ya Watu wa Uganda.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment