STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 19.10.2017
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein leo amemuapisha Kapteni Khamis Simba Khamis kuwa Naibu Mkuu
wa Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM).
Kapteni Khamis Simba
Khamis aliteuliwa hivi karibuni na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein kushika wadhifa huo.
Hafla hiyo,ilifanyika
Ikulu mjini Zanzibar ambayo imehudhuri na viongozi mbali mbali wa Serikali akiwemo
Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd, Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,
Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na
Katibu Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee.
Wengine ni Mkuu wa Mkoa
wa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed Mahmoud, Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh
Omar Kabih, Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman Ngwali, Wakuu wa Vikosi vya SMZ, Washauri wa Rais wa Zanzibar, Meya wa Manispaa
ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib pamoja na viongozi wengine wa
Serikali.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment