Habari za Punde

Msitu wa Popo wa Pemba Kivutio Kwa Watalii Wanaotembelea Kisiwani Humo.

Mmoja ya Hoteli za Kitalii Kisiwani Pemba inayotowa huduma kwa Wageni na Watalii wanaotembelea sehemu za historia katika Kisiwa hicho hupata huduma za malazi na maakuli katika Hoteli hii, Sehemu hii ni moja ya daraja la mbao hutumika katika hoteli hiyo ya Misali Sun Set Beach ilioko Wesha Wilaya ya Chakechake Pemba.  
Meneja wa Hoteli ya Kitalii ya Misali Sun Set Beach Pemba Zahran Juma akizungumza na mwandishi wa habari kutoka Unguja Salum Vuai akiwa katika kutembelea Utalii wa ndani kisimwani huo na kufika katika hoteli hiyo na kujionea maendeleo yake na huduma zinazotolewa kwa wageni na wanyeji wanaofika katika eneo hilo.
Mwandishi kutoka Idara ya Habari Maelezo Zanzibar Salum Vuai akiwa katika kutembeleo maeneo ya kitalii katika Msitu wa Hifadhi wa Popo wa Pemba akiwa katika ziara hiyo kujionea maendeleo ya Sekta ya Utalii Kisiwani Pemba. 
MWANDISHI wa habari wa kutoka Idara ya Habari Melezo Unguja, Salum Vuai Issa (nyuma), akiwa na dereva wa shirika la Magazeti ya serikali kisiwani Pemba, Ali Suleiman wakiingia kwenye hifadhi ya Popo wa Pemba, iliopo Kidike shehia ya Mjini Ole, wilaya ya Chakechake kisiwani humo.

MTEMBEZA wageni kwenye hifadhi ya Popo wa Pemba, iliopo kijiji cha Kidike shehia ya Mjini ole, Wilaya ya Chakechake, Omar Aminia Hamad, akionyesha baadhi ya machapisho kwenye ofisi yao, wakati waandishi wa habari walipofika kuitembelea hifadhi hiyo
MTENDAJI wa Hoteli ya Misali sun set beach iliopo Wesha wilaya ya Chakechake, ambae hakupatikana jina lake, akiwasha mashine ya kusukumia maji kwa wananchi wa shehia ya Wesha na hitelini hapo, ambapo kisima cha maji safi na salama kimechimbwa na uongozi wa Hoteli hiyo
MTENDAJI wa Hoteli ya Misali sun set beach iliopo Wesha wilaya ya Chakechake, ambae hakupatikana jina lake, akifungua mfereji ambao, upo karibu na kisima cha maji safi na salama, kilichochimba na uongozi wa hoteli hiyo, muda mfupi baada hya kuwasha mashine ya kisima hicho
KISIMA kilichochimbwa na uongozi hoteli ya Misali ya sun set beach iliopo Wedha wilaya ya Chakechake, ambacho kwa sasa pamoja na kwamba kinafanya kazi, lakini wananchi wa shehia ya Wesha ambao ndio wanufaika, hakijafanyiwa usafi na kuzungurukwa na majiani
(Picha na Haji Nassor , Pemba)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.