Habari za Punde

ZANTEL Yatoa Msaada wa Miamvuli 60 Kwa Chuo Cha Ustawi wa Jamii Jijini Dar es Salaam.

Meneja Mauzo wa Kampuni ya Mawasiliano ya Zantel, Jensen Msechu (kushoto) akisimika moja ya miamvuli iliyotolewa na Kampuni ya Mawasiliano ya Zantel kwa  Chuo cha Ustawi wa Jamii hivi karibuni jijini Dar es salaam.Jumla ya Miamvuli 60 ilitolewa kwa chuo hicho kwa lengo la kuwakinga jua wanafunzi wakati wa kujisomea wawapo chuoni hapo. Katikati ni Afisa Rasilimali watu Mwandamizi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Remidius Leonard na kulia ni Rais wa Wanafunzi, John Filimon.
Baadhi ya wanafunzi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii kilichopo eneo la Bamaga jijini Dar es salaam wakijisomea kwenye moja ya kizimba kilichosimikwa moja ya miamvuli iliyotolewa na Kampuni ya Mawasiliano ya Zantel hivi karibuni jijini Dar es salaam. Jumla ya miamvuli 60 ilitolewa kwa ajili ya kuwakinga jua Wanafunzi wa chuo hicho wakati wa kujisomea wawapo chuoni hapo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.