Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake Pemba, Rashid Hadidi Rashid, akizungumza na Wananchi wa kijiji cha Mtimbu Pujini , wakati ya ziara yake ya kuangalia changamoto zinazo wakabili Wananchi wa kijiji hicho.
PICHA NA JAMILA ABDALLA-MAELEZO PEMBA.
Na/Jamila Abdallah - Maelezo.
Serikali ya wilaya Chake
Chake , imesema itahakikisha inasaidia
na wananchi wa Kijiji cha Mtimbu Pujini katika kutatua changamoto ya elimu kwa
kushirikiana nao katika ujenzi wa
Skuli ya maandalizi kijijini
hapo.
Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa
Wilaya ya Chake Chake Pemba, Rashid Hadidi Rashid, alipokuwa akizungumza na
Wananchi wa kijiji hicho juu ya changamoto wanazokabiliana nazo ikiwa ni
miongoni mwa ziara zake za kuonana na Wananchi
katika shehia zao kuangalia mambo mbali mbali ya kimaendeleo.
Aliwataka wananchi wa kijiji cha Mtimbu Pujini kuunganisha nguvu za pamoja katika kuimarisha
maendeleo katika kijiji chao kwani maendeleo yao yataletwa na wao wenyewe.
Hadidi, alisema ni vyema wananchi
kushirikiana katika kujiletea maendeleo na kuachana na itikadi zao kwani
maendeleo hayawezi kuletwa na mtu mmoja bila mashirikiano ya pamoja.
"Mashirikiano yapamoja ndio
silaha pekee ya kuimarisha maendeleo ,hebu kuweni tayari tuweze kutatua
changamoto hizo hususan hii ya elimu", alisema Hadidi.
Aidha aliwahimiza wazazi kusimamia vyema masuala ya
elimu kwa watoto wao kwani elimu ndio mkombozi wao wa baadaye
na wakumbuke kuwa hakuna urithi mzuri kama kumuachia mtoto Elimu.
Kwa upande wao ,Wananchi wa kijiji
cha Mtimbu Pujini walisema mbali na changamoto mbali mbali wanazokabiliana nazo
wamekuwa wakilalamikia kukithiri kwa
watumiaji wa dawa za kulevya ambao huchangia wizi na uharibifu wa mazao.
Wananchi hao walisema kijiji cha Mtimbu sasa kimekuwa kukijitokeza
vitendo viovu ambavyo awali vilikuwa havipo kutokana na vijana kujiingiza
katika utumiaji wa dawa za kulevya.
Ali Kombo Masoud mkaazi wa Kijiji hicho , alisema kijiji
chao kimekuwa kikikabiliwa na changamoto nyingi, hivyo ameiomba Serikali ya
Wilaya kukisaidia kijiji hicho ili
kiweze kujiletea maendeleo na kuondosha changamoto zinazowakabili .
"Mtimbu ni kijiji kilichoko nyuma kimaendeleo hivyo tunaomba Serikali
utusaidie ili tuweze kujikwamua kimaendeleo na sisi"alisema Masoud.
No comments:
Post a Comment