STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar
29.01.2018

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein leo ameungana pamoja
na Wapiganaji wa Vikosi vya Ulinzi walioshiriki katika gwaride la kutimiza
miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar katika chakula cha mchana alichowaandalia
kutokana na ushiriki wao katika sherehe hizo zilizofanyika Januari 12 mwaka
huu.
Hafla hiyo ilifanyika
katika viwanja vya Makao Makuu ya KVZ, Mtoni mjini Unguja, na kuhudhuriwa na
viongozi mbali mbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar akiwemo makamo wa
Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd pamoja na Makamanda wa Vikosi vya
Ulinzi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania.
Katika shukrani zake
Dk. Shein kwa Wapiganaji hao zilizotolewa kwa niaba yake na Waziri wa Nchi
Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Issa Haji Ussi Gavu, alitoa pongezi kwa vikosi hivyo kwa kushiriki
kikamilifu katika sherehe hizo kutokana na gwaride zuri ambalo lilikuwa kivutio
kikubwa cha sherehe hizo zilizofanyika Januari 12, 2018 katika uwanja wa Amaan
mjini Unguja.
Waziri Gavu alitoa
shukurani na pongezi za dhati kwa vikosi hivyo kwa kuazimisha kwa hali ya juu
kilele cha miaka 54 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar ya Januari 12, 1964
ambazo zilifana kwa kiasi kikubwa.
Katika shukurani hizo,
Waziri Gavu alimpongeza Rais Dk. Shein kwa kuendeleza utamaduni wake wa
kuwaandalia chakula cha mchana wahusika wote kwa kufanya kazi kwa pamoja na
baadae kufurahi kwa pamoja kwa kula nao pamoja chakula cha mchana.
Waziri Gavu alieleza
kuwa hatua hiyo inaonesha wazi upendo mkubwa alionao Rais Dk. Shein kwa
wananchi wake kwa kufanya kazi kwa pamoja na baadae kufurahi kwa pamoja hali
ambayo imewapelekea vikosi hivyo kufarajika na hatua hiyo ya Rais.
Aidha, alivipongeza
kwa dhati vyombo hivyo vya ulinzi kwa kutekeleza majukumu yote waliyopangiwa
ikiwa ni pamoja na kuwalinda wananchi pamoja na mali zao sambamba na
kuhakikisha amani na utulivu inaimarishwa hapa nchini.
Pamoja na hayo, Waziri
Gavu alitoa wito kuendelea kuyalinda na kuyatunza Mapinduzi pamoja na kudumisha
uzalendo.
Ni utamaduni aliouweka
Dk. Shein wa kuwaandalia chakula cha mchana Vikosi vya Ulinzi vinavyoshiriki
katika gwaride la sherehe za Mapinduzi pamoja na vijana na wanafunzi ambao nao
hushiriki sherehe hizo kwa kila mwaka ambapo hapo jana aliwaandalia vijana na
wanafunzi walioshiriki katika maadhimisho ya Sherehe za kutimiza miaka 54 ya
Mapinduzi ya Zanzibar katika eneo hilo la viwanja vya Makamo Makuu ya KVZ,
Mtoni mjini Unguja
Rajab
Mkasaba, Ikulu
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment