Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, Azindua Kituo cha Afya Michezani Pemba Wilaya ya Mkoani.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiwasalimia Watoto walioandalia kwa ajili ya kumkaribisha katika Uzinduzi wa Kituo cha Afya Michezani Wilaya ya Mkoani Pemba kwa ajili ya kutowa huduma ya Afya kwa Wananchi wa Vijiji vya Wilaya hiyo ikiwa ni shamrashamra za Miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiondoa kipazia kuashiria Uzinduzi wa Kituo cha Afya Michezani Wilaya ya Mkoani Pemba.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akikata utepe kuashiria kukifungua rasmin Kituo cha Afya katika Kijiji cha Michezani Wilaya ya Mkoani Pemba, kulia Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Mahmoud Thabit Kombo.Uzinduzi huo umefanyika katika Kijiji hicho huko michezani Pemba.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mfanyakazi wa Kituo cha Afya Michezaji sehemu ya Chumba za Wazazi, Bi. Subira Ali Khamis, baada ya uzinduzi rasmin wa Kituo hicho kwa ajili ya kutowa huduma za Afya kwa wananchi wa sehemu hiyo na jirani.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Daktari Mohammed Faki Saleh baada ya kupokea maelezo ya huduma zinazotolewa na Katuo hicho.wakiwa katika sehemu ya mapokezi. 
Mfanyakazi wa Kituo cha Afya cha Michezani Hamad Sultani anayetoa huduma za dawa kwa wagonjwa wanaofika Kituo hapo akitowa maelezo kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, baada ya hafla ya kukifungua Kituo hicho cha Afya Michezani Wilaya ya Mkoani Pemba.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein na Waziri wa Afya Mhe. Mahmoud Thabit Kombo wakimsikiliza Mfanyakazi wa Kituo hicho Rajab Juma, akitowa  kwa Rais ya mgonjwa Rehema Omar, aliyelazwa katika chumba mapumziko.Kituo cha Afya Michezaji  
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiwasalimia Wananchi waliofika katika Kituo cha Afya cha Michezani kupata huduma ya matibabu baada ya kufunguliwa ikiwa ni shamrashamra za kuadhimisha Miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.











No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.