Habari za Punde

Waziri Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa Afungua Mkutano wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC) Jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Posta Tanzania (TPC), Dk. Haruni Kondo (wa pili kulia), akibadilishana mawazo na Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa TPC, Joseph Ngowi (kulia), wakati wakimsubiri mgeni rasmi, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa. Katikati ni Kaimu Postamasta Mkuu, Hassan Mwang'ombe.Wengine kushoto ni Maofisa waandamizi kutoka wizarani.
Kaimu Postamasta Mkuu, Hassan Mwang'ombe akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Shirika la Posta, ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, jijini Dar es Salaam leo. Wa pili kulia ni mgeni rasmi, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa.
Wajumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakisikiliza maelezo ya ufunguzi wa baraza hilo.   
Mwenyekiti wa Bodi ya TPC, Dk. Haruni Kondo akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri Profesa Mbarawa kuufungua mkutano huo. 
Baadhi ya Wajumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakisikiliza maelezo mbalimbali yaliyokuwa yakitolewa katika ufunguzi huo.
Baadhi ya Wajumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akifungua  mkutano huo. 
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Mbarawa, akizungumza na wajumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa TPC, wakati akiufungua mkutano wa baraza hilo, jijini Dar es Salaam leo. 
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Mbarawa, akizungumza na wajumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Posta. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Posta, Dk. Haruni Kondo na kulia ni Kaimu Postamasta Mkuu, Hassan Mwang'ombe. 
Baadhi ya wajumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi, wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Mbarawa.
Wajumbe wa Baraza Kuu, wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa.
Mjumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi, Peter Bihume, Meneja wa Posta Mkoa wa Kigoma, akimuuliza swali Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa katika mkutano huo.
Mjumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi, Ahmed Kaumo, ambaye pia ni Mwenyekiti TEWUTA, akitoa neno la shukrani kwa Waziri Prof. Mbarawa.
Mkuu wa Kitengo cha uhusiano cha TPC, Elia Madulesi, akizungumza, wakati akifafanua jambo katika mkutano huo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akisalimiana wajumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa TPC, mara baada ya kuufungua mkutano wao, jijini Dar es Salaam leo.  
 Mwenyekiti wa Bodi ya TPC Dkt. Haruni Kondo akisalimiana na wajumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi mara baada ya kuufungua mkutano wao huo jijini Dar es Salaam leo.
Wajumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi, wakiwa katika mkutano huo, leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa (katikati mbele), akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa TPC, mara baada ya kuufungua mkutano huo, jijini leo. kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Bodi ya TPC, Dk. Haruni Kondo na kulia kwake ni Kaimu Postamasta Mkuu, Hassan Mwang'ombe. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.