Baadhi ya meno ya viboko vipande 12,467 yenye uzito wa kilo 3,580.29 ambayo yameuzwa kwa njia ya mnada wa hadhara leo jijini Dar es Salaam kwa Kampuni ya On Tours Tanzania Limited kwa kiasi cha shilingi 30,900,000/= (Picha na Lusungu Helela- MNRT)
Serikali
kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa
Wanyamapori Tanzania (TAWA) imefanya mnada wa hadhara wa kuuza meno ya
viboko vipande 12,467 yenye uzito wa
kilo 3,580.29 katika ofisi zake ndogo katika Jengo la Mpingo, jijini Dar es Salaam ambapo jumla ya
makampuni 19 yenye leseni daraja la
kwanza yameshiriki katika mnada huo.
Mnada huo umefanyika chini ya usimamizi wa Wizara ya Fedha na
Mipango ambapo kampuni
ya On Tours Tanzania Limited imeibuka mshindi kwa kwa kununua meno hayo
kwa jumla ya shilingi 30,900,000/=
Awali akizungumza katika mnada huo, Mwenyekiti kutoka Wizara
ya Fedha na Mipango, Karerema Kwaleh aliwataka wafanyabiashara kuzingatia
masharti mnada huo.
Ambapo Karerema alimtaka mfanyabiashara yeyote atakeibuka mshindi kulipia asilimia ishirini na tano (25%) ya bei
papo hapo na asilimia sabini na tano (75%) italipwa yote katika muda wa siku
kumi na nne (14) baada ya mnada.
Kufuatia sharti hilo baada ya kutangazwa kwa mshindi,
Mwakilishi kutoka Kampuni hiyo,
Grey Kilas aliweza kulipia asilimia kiasi hicho cha asilimia ishirini na tano (25%) papo hapo na
asilimia sabini na tano (75%) atailipia ifikapo Februari 11, 2018.
Wakati huohuo, Mwakilishi
wa Mkurugenzi Mkuu TAWA, Mabula Misungwi amewatoa wasiwasi wananchi kuwa biashara hiyo haiwezi kuchochea ujangili kwa vile meno hayo yanauzwa kwa
wafanyabiashara wale tu
wenye leseni za nyara daraja la kwanza
Mabula amesema meno hayo yalianza kukusanywa tangu mwaka 2004 na huko nyuma
serikali ilikuwa ikiyauzia makampuni yenye leseni lakini kwa mwaka huo wameanza
utaratibu mpya wa kuuza meno hayo kwa njia ya mnada.
Kwa
upande wake Mwakilishi wa Kampuni hiyo, Grey Kilas ameishukuru wasimamizi wa
mnada huo kuwa umeendeshwa kwa uwazi wa hali ya juu na umetoa fursa kwa kila
mmoja wao
Akizungumzia
kuhusu soko, Kilasi amesema meno
hayo huuzwa nchini Japan, Marekani na Hongkong ambapo hutumika
katika kutengenezea mapambo kama vile stempu pamoja na vishikizo vya nguo.
Itakumbukwa
kuwa kwa mara mwisho biashara hiyo ya
kuuza meno ya viboko ilifanyika mwaka 2004.
No comments:
Post a Comment