Habari za Punde

Kampuni ya Pennyroyal Kupitia Mradi Wake wa Best of Zanzibar Kwa Kushirikiana na Internalional Volunteers Oman Yakabidhi Viti na Meza Kwa Skuli ya Sekondari na Msingi Kijini Matemwe Zanzibar.


Mkurungezi Mkuu wa Kampuni ya Pennyroyal Limited Brian Thomson , akikabidhi meza na viti 205 kwa Mkurugenzi wa Idara ya Elimu Msingi na Maandalizi Zanzibat Bi. Safia Rijal kwa ajili ya Skuli ya Sekondari na Msingi ya Kijini Matemwe, kupitia kitengo chake cha huduma kwa jamii Best of Zanzibar kwa kushirikiana na  International Volunteers Oman, hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Skuli hiyo Matemwe Wilaya ya Kaskazini A Unguja
Mkurungezi Mkuu wa Kampuni ya Pennyroyal Limited Brian Thomson , akikabidhi meza na viti 205,Mkurugenzi wa Idara ya Elimu Msingi na Maandalizi Zanzibat Bi. Safia Rijal, kwa ajili ya Skuli ya Sekondari na Msingi ya Kijini Matemwe, kupitia kitengo chake cha huduma kwa jamii Best of Zanzibar kwa kushirikiana na  International Volunteers Oman, hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Skuli hiyo Matemwe Wilaya ya Kaskazini A Unguja

Mkurungezi Idara ya Elimu Msingi na Maandalizi Bi. Safia Rijal akikabidhi moja ya meza na viti kwa ajili ya matumizi ya Skuli za Sekondari na Msingi za Kijiji cha Kijini Maatemwe na Wawakilishi wa International Volunteers Oman Hemed Mohammad, Danny Kim na Nahya Khamis wa Mradi wa Best Of Zanzibar, hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Skuli hiyo Matemwe Wilaya ya Kaskazini A, Unguja.
Mkurungezi Mkuu wa Kampuni ya Pennyroyal Limited Brian Thomson akiwa na Mwakilishi wa Internalional Volunteers Oman Danny Kim, wamekali meza na viti walivyokabidhi kwa Skuli za Sekondari na Msingi Kijini Matemwe Wilaya ya Kaskazini "A" Unguja, kulia Mkurugenzi Idara ya Elimu Msingi na Maandalazi Bi, Safi Rijal na Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Kijini Matemwe Mwalimu Ulimwengu Mkadam. hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Skuli hiyo Matemwe Kijini.
Mwakilishi wa Kampuni ya Pennyroyal Zanzibar Mohammed Issa akitowa maelezo kabla ya hafla ya makabidhiano wa vifaa kwa ajili ya Skuli za Sekondari na Msingi Kijini Matemwe Wilaya ya Kaskazini  "A" Unguja.
Mwakilishi wa International Volunteers Oman Danny Kim akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi Meza na Viti vyake 205, kwa Skuli za Sekondari na Msingi Kijiji cha Kijini Matemwe Wilaya ya Kaskazini "A" Unguja Skuli hizo zinapata ufadhili kupitia Mradi wa Bset of  Zanzibar, uliooko chini ya Kampuni ya Pennyroyal Zanzibar, inayojenga kijiji cha Utalii Matemwe Zanzibar. 
Mkurugenzi Idara ya Elimu Msingi na Maandalizi Zanzibar B. Safia Rijal akizungumza wakati wa hafla hiyoya kukabidhiwa Viti na Meza 205 kutoka kwa Mradi wa Best of Zanzibar kwa kushirikiana na Internalional Volunteers Oman, hafla hiyo ya makabidhiano imefanyika katika viwanja vya Skuli ya Sekondari Kijini Matemwe Wilaya ya Kaskazini "A" Unguja.na kuhudhuriwa na Wananchi wa kijiji hicho. 
Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Sekongari na Msini Kijini Matemwe Mwalimu Ulimwengu Mkadam akitowa neno la shukrani kwa msaada huo na kusema umefika wakati muwafaka.
Wazee wa Kijiji cha Kijini Matemwe Wilaya ya Kaskazini "A" Unguja wakifuatilia hafla hiyo ya makabidhiano ya Meza na Viti vyake 205 kwa ajili ya matumizi ya Skuli ya Sekondari na Msini Kijini Matemwe, hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Skuli hiyo Kijini. 



Mkurungezi Mkuu wa Kampuni ya Pennyroyal Limited Brian Thomson, akiwasalimia Wanafunzi wa Skuli ya Msingi Kijini baada ya hafla ya kukabidhi Meza na Viti vyake 205 kwa Mkurugenzi wa Idara ya Elimu Msingi na Maandalizi Zanzibat Bi. Safia Rijal kwa ajili ya Skuli ya Sekondari na Msingi ya Kijini Matemwe, kupitia kitengo chake cha huduma kwa jamii Best of Zanzibar kwa kushirikiana na  International Volunteers Oman, hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Skuli hiyo Matemwe Wilaya ya Kaskazini A Unguja


Pennyroyal Limited kupitia kitengo chake cha huduma kwa jamii Best of Zanzibar wakishirikiana na International Volunteers kutoka Oman wametoa msaada wa madawati 200 yenye thamani ya Tsh 18,000,000/- ( Shilingi millioni kumi na nane).
Akiongea katika sherehe za kukabidhiana, Mkurungezi Mkuu Bw. Brian Thomson alikua na haya ya kusema:

“Best of Zanzibar imejitolea kuboresha elimu katika shule za Kijini na Mbuyu Tende. Tumejiwekeza katika progamu tofauti za kielimu katika shule hizi mbili zikiwemu Masomo ya ziada (After Hours Tutoring program) kwa wanafunzi 500, na  kuwasomesha walimu 30 masomo ya lunga ya Kingereza na mbinu za kufundishia ili kuongeza uwezo na ujuzi wa walimu hao.

Tunawashukuru sana International Volunteers kwa moyo wao wa kujitolea na kushirikiana nasi katika kutoa huduma kwa mashule.”

Mkurungenzi huyo alisisitiza umuhimu wa elimu kwa maendeleo ya jamii na ukuwaji wa uchumi wa nchi,  ndio maana Best of Zanzibar imejikita katika uboreshaji wa elimu Zanzibar.

“Nia yetu kuu ni kuleta manufaa na kuedeleza msingi mzuri wa kiuchumi Zanzibar. Kwa muda mrefu sana watoto wa shule ya msingi Kijini na Mbuyu Tende wamekaa chini bila madawati kuwaletea ugumu katika kuelewa masomo na kupunguza ufanisi wao wa masomo.

Best of Zanzibar inashirikiana kwa ukaribu na Wizara ya Elimu katika kuboresha viwango vya elimu katika shule za Kijini na Mbuyu Tende. Na tunaishukuru sana Wizara ya Elimu kwa kutuunga mkono katika program zetu.” Aliongezea Bw. Brian Thomson.

Shule ya Kijini ina wanafunzi 903 na Mbuyu Tende inawanafunzi 603, katika wanafunzi hao 353 wanakaa chini bila madawati.

Mkurungezi wa Masomo ya Pre-Msingi na Msingi Wizara ya Elimu, Bi Safia Rajil alikua katika hafla hiyo  na alipongeza wawekezaji hao kwa msaada wao.

Kwa niaba ya Wizara ya Elimu napenda kutanguliza shukurani zetu za dhati kwa Best of Zanzibar na International Volunteers kwa kutoa madawati haya kwa shule hizi mbili. Msaasa huu utaleta madadiliko nakuongeza ufanisi wa watoto.”

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Kijini Bw. Ulimwengu Mkada Makame alishukuru sana kampuni ya Pennyroyal Ltd kwa msaada wao.

“ Shule yetu ilikua haina madawati kwa muda mrefu sana, tunashukuru Best of Zanzibar kwa kutukumbuka shule yetu.”

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.