Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.
Samia Suluhu Hassan amewataka wananchi wa mkoa wa Kaskazini Pemba kushirikiana
katika shughuli za maendeleo.
Makamu wa Rais ameyasema hayo wakati wa kuweka jiwe la
msingi la ujenzi wa kituo cha Afya cha Huduma ya Mama na Mtoto Shumba Vyamboni
wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba.
Kituo hicho cha Mama na Mtoto cha Shumba Vyamboni
kitatoa huduma za Mama na Mtoto ambapo jumla ya Wananchi 5,593 wakiwemo
wanawake wenye uwezo wa kuzaa 1543 na watoto chini ya umri wa miaka mitano 984
watapata huduma bora ya uzazi, lishe na ustawi wa mama na mtoto.
Vijiji vitakavyofaidika na huduma ya kituo hicho ni
pamoja na Kibubunzi, Kikunguni, Mihogoni, Nyuma ya Mti, Mgeninje, Utaani,
Shumba vya Mboni, Uwondwe, Mamoja, Gombe, Uwaani na Bule.
Katika ziara hiyo yenye lengo la kuhimiza shughuli za
maendeleo
Makamu wa Rais alikagua ujenzi wa Skuli ya Sekondari ya Micheweni
pamoja na kumtembelea Muasisi wa Chama Cha Mapinduzi Bi. Mrashi ambapo
alimkabidhi mabati ya kuezekea nyumba yake inayojengwa na wanachama wa chama
cha Mapinduzi katika eneo la Sizini.
Mwisho Makamu wa Rais aliweka jiwe la msingi la ujenzi
wa Tawi la CCM la Ukunjwi ambapo aliwaambia wakina Mama kuwa mstari wa mbele
katika kuonesha njia ya kuwa kiongozi bora.
No comments:
Post a Comment