Habari za Punde

NAIBU WAZIRI MAVUNDE AENDELEA KUWABANA WAAJIRI WANAOKIUKA SHERIA ZA NCHI

  NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Mkuranga
NAIBU Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde, ameendelea kuwabana waajiri wanaokiuka sheria za nchi ambapo leo Machi 8, 2018 amehamia wilayani Mkuranga Mkoa wa Pwani na kuvitoza faini ya jumla ya shilingi milioni 32, viwanda vitatu kwa  ukiukwaji mkubwa wa Sheria ya Kazi na Uhusiano Mahala pa Kazi.

Viwanda vilivyoadhibiwa ni pamoja na kiwanda cha kutengeenza yeboyebo cha Dorin Investment Company Limited, (milioni 14), LM Furniture, (milioni 7), na Tingtang, (milioni 14), adhabu hizo zimetangazwa leo Machi 8, 2018 na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde wakati wa ziara yake ya kushtukiza ili kubaini waajiri ambao wanakiuka sheria ya kazi na uhusiano kazini, na wale ambao bado hawajajisajili na Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF).

Kwa mujibu wa Naibu Waziri, viwanda hivyo vimekiuka sheria kwa kuhatarisha maisha na afya za wafanyakazi kutokana na mzingira hatarishi ikiwa ni pamoja na wafanyakazi kutokuwa na vifaa vya kujihami (protective gears), kufanya kazi masaa mengi bila ya kulipwa malipo ya muda wa ziada ambao uko nje ya muda wa kisheria wa mfanyakazi kufanya kazi.

Aidha Naibu Waziri ameagiza uongozi wa viwanda hivyo kuwasilisha nyaraka  muhimu kwa Kamishna wa Kazi, Jumatatu ijayo kwani nyaraka nyingi walizotakiwa kuzionyesha hawakuwa nazo, ikiwa ni pamoja na mikataba ya kazi, salary sleeps za wafanyakazi wao.

Sambamba na hilo Mheshimiwa Mavunde ameuagiza Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi (WCF), kumfikisha mahakamani mara moja mwajiri wa kiwanda cha kutengeneza vifaa vya plastiki, cha Tisino kwa kutojisajili na WCF kama sheria inavyotaka.

Naibu Waziri Mvunde yuko katika ziara ya kuwabaini waajiri ambao hawatekelezi ipasavyo Sheria ya Kazi na Uhusiano Kazini, na wale ambao bado hawajajisajili na Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF), na kuonya kuwa waajiri wote ambao bado hawajatekeleza takwa la kisheria la kujisajili WCF watapelekwa mahakamani na serikali haitabadili msimamo huo hadi hapo matakwa ya kisheria yatakapotekelezwa na waajiri wote nchini.

Naibu Waziri Mavunde, akizungumza na wafanyakazi wa kiwanda cha kutengeenza fanicha cha LM Furniture, ambapo aliwakuta wakifanya kazi katika mazingira hatarishi, wakiwa hawana vifaa vya kujihami, (protective gears).
 
 Naibu Waziri Mavunde akitoa maagizo kwa viongozi wa kiwanda cha kutengeenza viatu vya plastiki (yeboyebo), cha Dorin.
Naibu Waziri Mavunde, akizungumza na mmoja wa wafanyakazi wa kiwanda cha  LM Furniture ambaye licha ya kufanya kazi ya kuhamisha vitu vyenye ncha kali, kama vyuma na mabati hakuwa amevaa gloves, wala viatu vigumu (gumboots). Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF), Bi. Rehema Kabongo.
 Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani, Mhe. Filberto Hassan Sanga (katikati), akizungumza mbele ya Naibu Waziri Mvunde, na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano -WCF, Bi. Laura Kunenge.
 Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani, Mhe. Filberto Hassan Sanga (katikati), akizungumza mbele ya Naibu Waziri Mvunde, (wapili kulia), Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa WCF, Bi. Rehema Kabongo, (wakwanza kushoto) na Meneja wa kiwanda cha Tingtang, Bw. Lee.
 Wafanyakazi kiwanda cha Tingtang
  Wafanyakazi kiwanda cha Tingtang
  Wafanyakazi kiwanda cha Tingtang
 Mhe. Mavunde akimsikiliza Meneja wa kiwanda cha Tingtang, Bw. Lee.
 Wafanyakazi wa kiwanda cha Dorin, wakimsikilkzia Mhe. Mavunde, alipozungumza nao

 Maafisa wa juu waliofuatana na Mhe. Mavudne wakiwa pamoja na maafisa wa Idara ya Uhamiaji Wilaya ya Mkuranga.
Bw. Lee akijieleza mbele ya Mhe. Mavunde, na Kamishna wa Kazi, Bi. Hilda Kabisa,

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.