Baadhi ya Mawaziri waliohudhuria katika hafla ya kuapishwa Viongozi leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar ambapo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein aliwaapisha Viongozi hao Fatma Gharib Bilal kuwa Katibu Mkuu katika Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto na Nd,Abdalla Hassan Mitawi kuwa Naibu Katibu Mkuu katika Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais,[Picha na Ikulu,]28/03/2018.
Miongoni mwa Viongozi waliohudhuria katika kiapo cha Viongozi Fatma Gharib Bilal kuwa Katibu Mkuu katika Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto na Nd,Abdalla Hassan Mitawi kuwa Naibu Katibu Mkuu katika Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais,walioapishwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo,[Picha na Ikulu,] 28/03/2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais Mhe.Balozi Seif Ali Iddi kabla kuwaapisha Viongozi aliowateuwa hivi karibuni hafla hiyo ya kiapo ilifanyika leo ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar,[Picha na Ikulu,] 28/03/2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Fatma Gharib Bilal kuwa Katibu Mkuu katika Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto katika hafla iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar,[Picha na Ikulu,] 28/03/2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Nd,Abdalla Hassan Mitawi kuwa Naibu Katibu Mkuu katika Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais katika hafla iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar,[Picha na Ikulu,] 28/03/2018.
STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 28.03.2018
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein leo amewaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni kushika nyadhifa
mbali mbali katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Viongozi walioapishwa
na Rais Dk. Shein katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar ni Fatma Gharib
Bilal ambaye ameapishwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee,
Wanawake na Watoto.
Mwengine aliyeapishwa
ni Abdalla Hassan Mitawi kuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamo wa Pili wa
Rais.
Hafla hiyo, ilihudhuriwa
na viongozi mbali mbali akiwemo Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali
Maulid, Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar
Othman Makungu, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said pamoja na Mawaziri.
Viongozi wengine
waliohudhuria hafla hiyo ni Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabih, Kadhi
Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji, Mkuu wa
Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed Mahmoud, Washauri wa Rais wa
Zanzibar pamoja na viongozi wengine wa Serikali.
Katika maelezo yao
viongozi hao mara baada ya kuapishwa waliahidi kutekeleza majukumu yao kwa
mashirikiano ya pamoja kati yao na viongozi wengine wote wa Serikali wakiwemo
wale wa Wizara zao pamoja na Ofisi watakazoziongoza.
Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
Postal Address:
2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment