Habari za Punde

Uongozi wa HUAWEI Wazungumza na Rais wa Zanzibar Dk. Shein Ikulu Zanzibar leo.


Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akizungumza na Ujumbe wa Huawei unaoongozwa na  Mkurugenzi Mkuu wa Huawei Bw.Gao Mengdong (wa pili kulia)  ujumbe huo ulipofika Ikulu Zanzibar  leo kwa mazungumzo. [Picha na Ikulu.]

Rais Dk. Shein alifanya mazungumzo na ujumbe wa Kampuni ya Mawasiliano ya HUAWEI kutoka China chini ya uongozi wa Mwenyekiti wa Kampuni hiyo tawi la Tanzania  Gao Mengdong, Ikulu mjini Zanzibar.

Dk. Shein aliipongeza Kampuni ya HUAWEI kwa kuendeleza mawasiliano ya kisasa kwa kuanzisha simu zenye mfumo wa kisasa wa 5G pamoja na kueleza maendeleo ya miradi yao kwa Zanzibar pamoja na mchakato wa mradi wa umeme wa kutumia jua.

Nao uongozi huo wa HUAWEI ulimuahidi kuwa Kampuni yao iko tayari kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha Teknolojia ya Habari na Mawasilaino pamoja na kuutumia uzoefu wake wa miradi ya umeme wa kutumia jua.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.