Habari za Punde

UVCCM Wete watakiwa kuanzisha vikundi vya ushirika


Na Said Abdulrahman Pemba.

WANACHAMA wa jumuia ya Umoja wa Vijana wa CCM Wilaya ya Wete. wametakiwa kujikusanya pamoja na kuanzisha vikundi vya ushirika katika matawi yao na kuacha kutegemea ajira Serikalini.

Akizungumza na wanachama hao katika ukumbi wa Ofisi ya CCM Wilaya ya Wete,Katibu hamasa kutoka Wilaya ya Kati Unguja, Ali Khamis Suleiman, alisema Serikali ulimwenguni kote hazina uwezo wa kuajiri raia wake wote isipokuwa hufatafutia mbinu mbali mbali za kujiajiri.

Alifahamisha kuwa tatizo kubwa ambalo lipo katika visiwa hivi ni ukosefu wa  ubunifu wa miradi ya maendeleo ila ajira zipo nyingi tu wafanyakazi wa kazi hizo hawapo.

Alieleza kuwa vijana ndio nguvu kazi ya taifa hili na ndio maana Serikali zote mbili zikawa zinatoa fursa kwa vijana wake.

“Sisi vijana ndio wakuleta maendeleo katika taifa hili,na  kama sisi tutaamua kufanya vitendo vinavyoweza kuharibu amani ni sisi,”alisema Katibu huyo.

Sambamba na hayo Katibu Ali, aliwataka wanachama hao kuachana na ile CCM ya zamani ya iyena iyena tu bali ni kufanya kazi kwa uzalendo na kusimamia vyema ilani ya Chama hicho.

Aidha waliwataka wanachama hao kukitetea Chama chao na kutoa hoja pale ambapo itabidi na kuwaeleza kuwa wasifanye makosa ambayo walifanya katika uchaguzi wa mwaka 2015.

Nao baadhi ya wajumbe wa mkutano huo  walieleza kuwa tatizo kubwa ambalo lipo katika maeneo yao ni kutokuwa na mashirikiano na masheha wa shehia zao kwani wamekuwa wakiwadharau na kutowajali.

Aliutaka uongozi wa Umoja huo kukaa pamoja na Masheha wote wa Shehia zilizomo ndani ya Wilaya ya Wete ili kuwapa darasa ambalo litaweza kuondosha lawama juu yao.

“Licha ya yote hayo ila pingamizi kubwa ambayo tunakabiliana nayo wakati tukiwa na matatizo yetu ni masheha kwani tunapowaendelea na shida zetu wanatuambia sisi hawatufahamu,”walisema wajumbe hao.

Hivyo walisema wamepokea ujumbe huo na wako tayari kukaa pamoja na kujikusanya kwa lengo la kufanyakazi za kujiletea maendeleo yao.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.