Habari za Punde

Walimu watakiwa kuzingatia sheria na kanuni za utumishi

 Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Nd. Salim Kitwana Sururu akifungua mafunzo ya siku mbili kwa waajiriwa wapya (walimu) Katika Ukumbi wa Baraza la Mji Chachani Chake Chake Pemba tarehe 24-25/03/2018
 Afisa Mdhamini Wizara ya Nchi Ofisi ya Raisi Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala bora Ndugu Massoud Ali Moh’d akifunga mafunzo ya siku mbili kwa waajiriwa wapya (walimu) Katika Ukumbi wa Baraza la Mji Chachani Chake Chake tarehe Pemba 24-25/03/2018
 Mratibu wa Taasisis ya Elimu Bi Asha Soud Nassor akiwasilisha mada kuhusu mitaala katika mafunzo ya siku mbili kwa waajiriwa wapya (walimu) Katika Ukumbi wa Baraza la Mji Chachani Chake Chake Pemba tarehe 24-25/03/2018
 Mrajisi Bi Hidaya Omar Khamis akiwasilisha mada kuhusu miiko na maadili ya Ualimu katika mafunzo ya siku mbili kwa waajiriwa wapya (walimu) Katika Ukumbi wa Baraza la Mji Chachani Chake Chake Pemba tarehe 24-25/03/2018

Washiriki wa mafunzo (walimu) wakiwa katika Ukumbi wa Baraza la Mji Chachani Chake Chake Pemba.


Na Ali Othman Ali, Pemba

Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mh. Salim Kitwana Sururu amewataka wakaguzi kuwafuatilia kwa karibu walimu walioajiriwa hivi karibuni ili kuhakikisha kwamba wanafanya kazi kwa ufanisi.

Akifungua mafunzo ya siku mbili kwa walimu 82 waliojiriwa hivi karibuni katika ukumbi wa baraza la mji Chachani Chake Chake Pemba, Mh. Sururu amewataka walimu hao kulinda heshima na kujipatia umaarufu kwa kufundisha kwa bidii na kujifunza zaidi.

Kwa upande wake Mratibu wa Taasisis ya Elimu Bi Asha Soud Nassor akiwasilisha mada kuhusu mitaala aliwataka walimu kufundisha kwa kutumia vifaa na teknolojia badala ya kutumia kitabu cha mwanafunzi pekee.

Kwa upande wake Mrajisi Bi Hidaya Omar Khamis ameawataka walimu hao kuielewa sharia ya elimu namba 6 ya mwaka 1982, kanuni za miiko na maadili ya kazi ya ualimu chini ya kifungu cha 59 (1) (Z).

Akifafanua kanuni hiyo Bihidaya amesema Mtu yeyote anaetaka kuajiriwa katika kazi ya ualimu atalazimika kuliridhisha baraza la elimu kwamba pamoja na sifa za kielimu anao mwelekeo wa kua mwalimu muadilifu.

Bi Hidaya ameongeza kwamba niwajibu kwa kila mwalimu kufuata miiko ya ualimu wakati wote akiwa ndani na nje ya skuli.

Nae Afisa Mdhamini Wizara ya Nchi Ofisi ya Raisi Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala bora Ndugu Massoud Ali Moh’d akifunga mafunzo hayo amewataka walimu hao kufanya kazi kwa kuzingatia sharia na kanuni za Utumishi wa Umma na kuacha mambo yote yanayokwenda kinyume na sharia hiyo.

Nd. Masoud amewasihi walimu hao kutambua nafasi yao kama watumishi wa umma hivyo hawana budi kutii serikali na viongozi waliopo madarakani ikiwa ni moja ya kanuni katika sharia ya Utumishi.

“Sharti jengine kwa mujibu wa kanuni hii nilazima mtumishi wa umma aheshimu viongozi na Serikali iliokuwepo madarakani, mkono unaokulisha usiutemee mate” Alisisitiza Nd. Moh’d.

Jumla ya walimu 82 walioshiriki mafunzo hayo wameshaanza kazi katika skuli mbali mbali kisiwani Pemba na kupunguza tatizo la uhaba wa walimu katika skuli za serikali.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.