Waziri wa Habari
Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akizungumza na
waandishi wa habari (hawapo pichani) baada ya kufanya kikao na wasanii wa mziki
Roma Mkatoliki na Pretty Kind jana jijini Dar es Salaam. Pembeni kwa waziri ni
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza
Naibu Waziri wa
Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kulia) akifafanua jambo
wakati wa kikao na waandishi wa habari baada ya kufanya mazungumzo na wasanii Roma
Mkatoliki na Pretty Kind jana Jijini Dar es Salaam. Katikati ni mwakilishi
kutoka Bodi ya Filamu Bw. Benson Mkenda na kushoto ni msanii wa mziki Pretty
Kind
Naibu Waziri wa
Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kushoto) akiwaonyesha
waandishi wa habari nakala ya cheti cha usajili cha msanii Pretty Kind kutoka
BASATA wakati wa kikao na waandishi wa habari jana Jijini Dar es Salaam. Kulia
ni Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe
Msanii wa mziki wa
bongo fleva Roma Mkatoliki (kulia) akizungumza na waandishi wa habari jana
Jijini Dar es Salaam baada ya kufanya kikao na Waziri pamoja na Naibu Waziri
ambapo alitangaza kuufuta na kuviomba vyombo vya habari kutoucheza tena wimbo
wake wa kibamia. Kushoto ni Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA)
Bw. Godfrey Mngereza
Msanii wa mziki wa
bongo fleva Pretty Kind (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari jana
Jijini Dar es Salaam baada ya kufunguliwa kifungo alichokua amefungiwa cha
kutojihusisha na mziki kwa miezi sita na kuahidi kuwa balozi mwema wa maadili
kwa wasanii wenzake. Kulia ni Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo
Mhe. Juliana Shonza
Mwakilishi kutoka Bodi ya Filamu Bw. Benson Mkenda (kulia) akifafanua jambo
wakati wakati wa kikao na waandishi wa habari baada ya kuzungumza na wasanii
Roma Mkatoliki na Pretty Kind jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri wa
Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe katika
picha ya pamoja na Msanii Roma Mkatoliki (wapili kushoto) na msanii Pretty Kind
(kulia) baada ya kuzungumza nao na kurekebisha tofauti zilizopelekea kufungiwa
kwa wasanii hao jana Jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Naibu Waziri wa
Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza
Picha
na:
Genofeva Matemu - WHUSM
Na: Genofeva Matemu –
WHUSM. 30/03/2018
Waziri wa Habari
Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amemtaka Msanii wa
muziki wa bongo fleva Roma Mkatoliki kujisajili BASATA ili aweze kuondolewa
kwenye kifungo chake cha kutokufanya shughuli za sanaa kwa miezi sita
alichofungiwa mwanzoni mwa mwezi machi mwaka huu.
Hayo ameyasema wakati
wa kikao na waandishi wa habari jana Jijini Dar es Salaam baada ya kikao na
wasanii wa mziki Roma Mkatoliki na Pretty Kind ambapo Wizara ilimtaka msanii
Roma kubadilisha wimbo wake wa kibamia na kujisajili BASATA ili aweze
kuondolewa katika kifungo hicho ambapo msanii huyo alitangaza kuufuta wimbo huo
na kuahidi kujisajili BASATA ili aweze kuendelea na mziki.
“Kwa kuwa msanii Roma
Mkatoliki ameamua kuufuta kabisa wimbo wa kibamia na kuvitaka vyombo vya habari
kutokuucheza tena wimbo huo Wizara inamfungulia kifungo chake mara tu baada ya
kujisajili BASATA atakuwa huru kuendelea na kazi zake za sanaa” amesema Mhe.
Mwakyembe
Aidha Naibu Waziri
Shonza amesema kuwa Msanii Suzan Michael (Pretty Kind) ametambua kosa alilolifanya
na kukiri kosa hilo kwa kufanya jitihada mbalimbali ikiwemo kuandika barua ya
kuomba msamaa na kujisajili BASATA kuwa msanii halali hivyo Wizara kwa
kushirikiana na BASATA imeridhia kumfungulia adhabu aliyopewa ya miezi sita
ambayo kimsingi ilitakiwa kuisha tarehe moja julai mwaka huu.
“Kuanzia sasa msanii
Pretty Kind yupo huru kuendelea na kazi zake za sanaa kutokana na yeye kutimiza
matakwa aliyoagizwa kuyafanya na kuahidi kuwa balozi mwema wa masuala ya
maadili kwa wasanii wenzake” amesema Mhe. Shonza
Hali kadhalika Mhe.
Shonza amewaomba wasanii wengine nchini kuiga mfano wa msanii Pretty Kind wa
kujisajili BASATA ili waweze kutambulika rasmi katika tasnia ya sanaa na kuweza
kuendana na sheria, kanuni na taratibu zilizopo katika tasnia hiyo kwa maslahi
yao na taifa kwa ujumla.
Naye msanii wa muziki
nchini Roma Mkatoriki ameviomba vyombo vya habari nchini kuufuta, kuuondoa
sokoni na kuacha kuucheza wimbo wake ujulikanao kwa jina la kibamia kwani wimbo
huo umekua ukileta ukakasi katika jamii kutokana na maneno pamoja na picha
jongevu zilizotumika katika wimbo huo.
Sanjari Msanii
chipukizi wa bongo fleva Bi. Suzan Michael (Pretty Kind) ameishukuru Wizara ya
Habari kwa kuweza kumweka sawa na kwenye mstari ulionyooka kwa kufuata taratibu
za kujisajili kwani sanaa ni kazi kama vile zilivyo kazi zingine hivyo kuwaomba
wasanii wenzake kubadilika na kusimamia ndoto zao ili waweza kuleta sifa nzuri
kwa nchi ya Tanzania.
No comments:
Post a Comment