Habari za Punde

Barabara ya Mkoani Chake yaharibika tena eneo la Changaweni kutokana na mvua za Masika

 ENEO Changaweni la barabara ya Mkoani- Chake chake Pemba, ambalo limeharibika tena kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha, ambapo mwezi Mei mwaka jana, pia eneo liliharibika na kujengwa bila ya mafanikio, ambapo kwa sasa wizara ya ujenzi Pemba, imerejea kuitengeneza kipande cha barabara yake za zamani, na ndio wananchi wanapotumia kwa sasa, (Picha na Haji Nassor).
 FOLENI ya gari baadhi yao zilizobebea mizigo ya abiria walioshuka meli wakitokea Unguja, ambapo walilazimika kukaa eneo la Changaweni Mkoani kwa saa mbili, kufuatia barabara kuharibika na eneo lililoruhusiwa kupita kwa dharura, nayo gari ya mzigo inayodaiwa ni ya Kampuni ya Azam kukwama, (Picha na Haji Nassor).
 MOJA ya gari za abiria aina ya Dyna, inayofanya kazi zake Mkoani-Chakechake, ikivutwa na gari la kijiko, baada ya kukwama eneo ambalo pia gari ya mzigo inayodaiwa kuwa ni ya Kampuni ya Azam, kukwama na kusababisha foleni, iliodumu kwa saa mbili, eneo la Changaweni Mkoani, ambapo barabara ya kawaida iliharibi kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha, (Picha na Haji Nassor).

GARI ya mzigo inayodaiwa kuwa ni kampuni ya Azam, ikiwa imeshatolewa na gari la kijiko, ambapo gari hiyo ilikwama eneo la barabara ya dharura hapo Changaweni Mkoani, na kusababisha, abiria waliokuwa wakitokea Unguja na wengine Chake chake, kukwama kuanzia saa 10:00 jioni hadi 12:44, (Picha na Haji Nassor).  

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.