RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed
Shein amewahimiza wananchi wa Zanzibar na Watanzania wote kwa jumla kuyatumia
mafunzo ya mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa kuendeleza umoja, upendo na mshikamano
walionao.
Akitoa neno la shukurani kwa niaba ya Rais,
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekitiwa Baraza la Mapinduzi Issa Haji Gavu
aliyasema hayo katika futari maalum iliyoandaliwa na Rais kwa ajili ya wananchi
pamoja na viongozi mbali mbali wa dini, vyama vya siasa na serikali,
iliyofanyika kwenye viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar.
Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi
Seif Ali Idd alihudhuria ambapo Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein
nae kwa upande wake aliungana pamoja na wananchi wa Mkoa huo pamoja na viongozi
mbali mbali wanawake wa kitaifa katika futari hiyo maalum.
Dk. Shein alieleza imani yake kuwa umoja,
upendo na mshikamano uliopo nchini iwapo utaendelezwa utaweza kuleta faida
kubwa kwa wananchi wote pamoja na vizazi vijavyo.
Alhaj Dk. Shein alitoa shukurani kwa waalikwa
wote waliofika katika hafla hiyo kwa kuitikia wito na mwaliko wake huo wa kuja
na kutimiza kitendo cha kufutari kwa pamoja.
Aliongeza kuwa shughuli hiyo ni
mwendelezo wa kufutarisha wananchi wote wa Unguja na Pemba katika futari maalum
anazoziandaa Alhaj Dk. Shein kwa ajili ya wananchi hao pamoja na viongozi mbali
mbali ambao hufutari nao pamoja.
Aidha, Alhaj Dk. Shein aliwatakia kila la
kheri wananchi wote Zanzibar na Tanzania kwa jumla katika kukamilisha mwezi
Mtukufu wa Ramadhani na kuwasisitiza kuendelea kuiombea dua nchi na wale ambao
watajaaliwa kumaliza salama mwezi huo mtukufu
aliwatakia Idd njema na yenye baraka tele.
Dk. Shein alianza ziara za kuwafutarisha
wananchi pamoja na viongozi katika mikoa yote ya Zanzibar katika ziara
zilizoanza kwenye Mkoa wa Kaskazini Pemba huko katika viwanja vya Ikulu ndogo
ya Michweni mnamo Juni 5, 2018 sawa na mwezi 20 Ramadhan na kumalizia jana
katika Mkoa huo wa Mjini Magharibi hapo katika viwanja vya Ikulu ya Zanzibar.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024
2231822
E-mail:
rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment