Habari za Punde

TAMUFO Yazionya Kampuni za Kuuza Muziki Nchini Kenya.


Wadau wa muziki kutoka Tanzania na Kenya wakiwa katika mkutano na  viongozi wa Umoja wa Wanamuzi Tanzania (TAMUFO), ulioshirikisha vikundi mbalimbali vya Kwaya ili kuwajengea uelewa na kuhakikisha wanafaidika na kazi zao za muziki unaoendelea jijini Arusha. Kushoto mbele mwenye tai ni Rais wa TAMUFO Dk. Donald Kisanga.
 Majadiliano yakiendelea.


Na Dotto Mwaibale
UMOJA wa Wanamuziki Tanzania (TAMUFO) umeyataka makampuni ya Kenya yanayouza nyimbo za wanamuziki wa Tanzania bila kufuata utaratibu kuacha kufanya hivyo mara moja.

Ombi hilo limetolewa na Rais wa TAMUFO Dk.Donald Kisanga mjini Arusha juzi wakati  viongozi wa TAMUFO walipofanya mkutano na Vikundi mbalimbali vya Kwaya ili kuwajengea uelewa na kuhakikisha wanafaidika na kazi zao za muziki na kuwaunganisha na fursa za Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa gharama nafuu kupitia  umoja huo.

"Natoa onyo kali kwa makampuni ya Kenya yanayouza nyimbo zilizoimbwa na watanzania na kurekodiwa na Tanzania kuuzwa kenya Kinyume cha Taratibu na kuwakosesha wanamuziki wa Tanzania Kufaidika na kazi zao na serikali kukosa mapato kupitia kodi" alisema Kisanga
Alisema katika mkutano huo Kampuni ya Kenya ya Africha ilikiri kosa na Kuahidi kuwalipa Wanamuziki  Wa Tanzania Pesa zao bila masharti yoyote baada ya kiziuza bila ya kufuata taratibu na kuwa TAMUFO na kampuni hiyo watatiliana saini za makubaliano kwenye mkutano huo. 

Katibu Mkuu wa TAMUFO, Stellah Joel alivitaja Vikundi vilivyohudhuria mkutano huo kuwa ni Kwaya Kuu Habari Njema na Kwaya ya UinjilistI za Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Mjini kati Arusha, Kwaya kongwe za Ulyankulu Mapigano na Ulyankulu Barabara ya 13 zote za Tabora.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.