Habari za Punde

Arsenal yapata ushindi wa kwanza huku ManCity ikizuiwa na Wolveshampton

Arsenal ilirekodi ushindi wake wa kwanza katika ligi ya Premia chini ya mkufunzi mpya Unai Emery baada ya bao la kujifunga la Issa Diop na bao la dakika za lala salama la Danny Welbeck kuilaza West ham.
Arsenal ambayo imekuwa na safu ya ulinzi inayoyumbayumba ilitoka nyuma na kuongoza baada ya krosi ya Lacazette kumgonga Diop na kuingia.
Hector Bellerin baadaye alimuona Wellbeck ambaye alikuwa pekee katika lango la West Ham dakika za lala salama ambaye alicheka na wavu.
Nahodha wa West Ham Marko Arnautovic aliwaweka mbele wageni hao baada ya dakika 25, baada ya kupata pasi nzuri kutoka kwa felipe Anderson kabla ya kumfunga kipa Cech.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.