Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) Bi. Sabra Issa Machano akitowa maelezo ya Kitaalamu ya Ujenzi Mkubwa wa Jengo la Treni Darajani (Chawl Building Darajani)leo 14 AGOSTI, 2018
MHE. RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA
MAPINDUZI – DR. ALI MOHAMED SHEIN
MH. MAKAMO
WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR, BALOZI SEIF ALI IDDI
MHESHIMIWA
JAJI MKUU WA ZANZIBAR, OMAR OTHMAN MAKUNGU,
MHE. SPIKA
WA BARAZA LA WAWAKILISHI, ZUBEIR ALI MAULID
MH. WAZIRI
WA FEDHA NA MIPANGO, DKT KHALID SALUM MOHD
WAHESHIMIWA
MAWAZIRI WA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR
MHESHIMIWA MKUU WA MKOA WA MJINI MAGHRIBI, AYOUB
MOHAMMED MAHMOUD,
WAHESHIMIWA WAKUU WA MIKOA.
WAHESHIMIWA WAWAKILISHI,
WABUNGE NA
VIONGOZI WOTE WA SERIKALI NA VYAMA VYA SIASA.
MAKATIBU
WAKUU WA WIZARA ZA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR,
MWENYEKITI
NA WAJUMBE WA BODI YA WADHAMINI YA MFUKO WA HIFADHI
WAKURUGENZI
NA VIONGOZI WA SERIKALI
WAHESHIMIWA MABIBI
NA MABWANA
ASALAM ALEYKUM;
Awali
ya yote napenda kuchukuwa nafasi hii adhimu
kumshukuru Allah Subhannahu Wataala
kwa kutujaalia afya njema na kutuwezesha
kushiriki katika sherehe hizi za uzinduzi rasmi wa Chawl Building au
kama linavyofahamika na wengi “Jumba la Treni” baada ya matengenezo yaliyochukua
takriban miezi ishirini ikiwa ni sawa na
mwaka mmoja na miezi minane.
Shukurani
za pili zije kwako Mh. Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein kwa kukubali kwako kuwa mgeni wetu rasmi wa shughuli hii.
Tuna furaha kubwa kuwa nawe kwani
tunafahamu majukumu mazito na ratiba ngumu uliyo nayo ukiwa ni Kiongozi wetu na Mkuu wa Nchi hii.
Pia,
nitoe shukurani zangu tena kwako kwa ushauri wako pamoja na maelekezo mbalimbali uliyotupatia, maelekezo
ambayo lengo lake yalikuwa katika
kuhakikisha ZSSF inatekeleza majukumu yake kwa ufanisi na mafanikio makubwa
katika matengenezo haya, ili ZSSF iweze
kuchangia kwa kiasi katika kuleta maendeleo kwa nchi na wananchi wake. Lakini
pia kwa kuwapatia wafanyabiashara mazingira mazuri ya kufanyia shughuli zao baada ya kukamilika kwa matengenezo makubwa ya
jengo mashuhuri la chawl (jumba la treni).
Shukurani
nyengine ni kwa Makamo wa Rais wa Zanzibar Mh. Balozi Seif Ali Idd ambae mbali
ya ushauri wake wenye dira lakini alikuwa nasi bega kwa bega tokea katika vikao
mbalimbali lakini pia amefanya ziara kadhaa kuangalia hatua zinavyoendelea na
kutupa ushauri wake ulioonesha ubobezi wake katika uongozi na maendeleo kwa
ujumla, Shukurani Mh. Balozi Seif Ali Idd.
Mh.
Mgeni Rasmi
Naomba
sasa kwa heshima na unyenyekevu mkubwa uniruhusu,
nitoe taarifa fupi ya mradi huu wa jengo la chawl maarufu kama jumba la treni.
Jengo
la Chawl ambalo Shirika la UNESCO wanalitambua kama ni jengo la zamani ‘grade
A’ awali lilijengwa na Sultan Barghash Mwaka 1880. Alilijenga ili lisaidie
kukuza biashara katika mji huu lakini pia kusaidia kuchangia huduma za maji mji
mkongwe lakini pia katika misikiti iliyowekwa wakfu katika mji huu kwa huduma
mbalimbali.
Lilijengwa
kwa kutumia boriti, mawe, udungo na chokaa na lilikuwa karibu na daraja
lililounganisha sehemu mbili. Kutokana na kupitiwa na zaidi ya miaka mia moja
jengo hili lianza kuchakaa.
Hata hivyo kutokana
na umuhimu wake kijamii, kitalii na taswira yake katika mji mkongwe Serikali
kupitia Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati ilikabidhi kwa Mfuko wa
Hifadhi ya Jamii-Zanzibar jengo hili mnamo mwezi Juni 2016 ili kulifanyia matengenezo.
Awali,
Kazi ya kulifanyia marekebisho ilikabidhiwa kwa Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji
na Nishati chini ya usimamizi wa Shirika la Nyumba (ZHC) na Mamlaka ya Uhifadhi
na Uendelezaji wa Mji Mkongwe (STCDA) na hasa ukizingatia kuwa jengo hilo lipo
ndani ya eneo la Mji Mkongwe na lina hadhi ya daraja la kwanza la uhifadhi wa
kimataifa.
Mfuko
wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar ulitakiwa kutoa fedha za mradi huo baada ya kuona
kuwa mradi unaweza kujiendesha kibiashara na kukabidhiwa rasmi usimamizi wa
mradi huo na umiliki wa jengo tarehe 6 Agosti 2015 kwa lease ya miaka sitini na
sita (66), na kukabidhiwa rasmi Juni 2016 kuwa wamiliki wa jengo.
Mh
Mgeni Rasmi
Kutokana
na kuwa jengo hilo lilikuwa na wapangaji tofauti waliokuwa wakiishi na wafanyabiashara katika milango mbalimbali
ya maduka, Wizara ya Ardhi kwa kushirikiana na Kamati ya mawaziri watano
walifanya kikao na wafanyabiashara hao na wakaazi kwa kuwafahamisha azma na lengo la Serikali na kuwataka kuhama ili
kupisha ukarabati, Pia ulazima wa wapangaji hao kuhama ulitokana na hali ya
ubovu wa jengo wakati huo.
Hivyo,
Wafanyabiashara hao walihama mnamo tarehe 5 Juni 2016 ili kupisha ujenzi wa
jengo. Katika kufikia lengo la mradi Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar
ulichukua hatua zifuatazo:-
·
Kuzungusha
mabati eneo lote la mradi "hoarding" ili kuzuia wizi na uharibifu wa
jengo pamoja na kuweka ulinzi wa kikosi cha Valantia.
·
Kutoa
zabuni ya ushauri elekezi na kufanikiwa kuipata kampuni ya CONS AFRICA ya
Dar-es-Salaam kuifanya
kazi hiyo. Kampuni hiyo ilifanya kazi kwa karibu sana na Mamlaka ya
Uhifadhi na uendelezaji wa mji mkongwe (STCDA) ikiwa ni pamoja na kutoa
miongozo na kuhakikisha kazi inaenda kwa mujibu wa taratibu na sheria za Mji
Mkongwe.
·
Kushirikiana
na Mamlaka ya Uhifadhi (STCDA) michoro iliochorwa na mshauri elekezi iliwasilishwa
UNESCO kwa ajili ya kupata ridhaa ya ujenzi. UNESCO walitoa ridhaa ya kuendelea
na ujenzi baada ya kufanya ziara katika mradi huo mwezi Oktoba 2017 [k1] pamoja na kutoa maelekezo machache ambayo mshauri
na mkandarasi aliyafanyia kazi.
·
Kutoa
zabuni za mkandarasi mkuu (Main Contractor) na wakandarasi wadogo
(Sub-Contractor), kampuni zilizofanikiwa kushinda kazi za ujenzi CRJE
(EA) LTD – kama mkandarasi
mkuu kwa gharama ya TZS 8.4 bilioni. CRJE (EA) LTD – pia
akiwa mkandarasi mdogo wa huduma za maji safi, maji machafu na huduma za
kujikinga na moto (Plumbing and Fire fighting) kwa gharama ya TZS 613,555,632.
Gesap engineering group limited - mkandarasi mdogo
wa huduma za Umeme
(Electrical) kwa gharama ya TZS 984,374,998. Gesap engineering
group limited - mkandarasi mdogo wa huduma
za "ICT"
kwa gharama ya TZS 292,908,332. Derm Elevators Limited
- mkandarasi mdogo wa huduma za "Lifti"
kwa gharama ya TZS 652,851,179. CITCC (Tanzania)
Limited - mkandarasi mdogo wa huduma
za "Air Condition"
kwa gharama ya TZS 733,861,508 Gharama
za mradi hadi kukamilika kwake zinatarajiwa kuwa ni TZS 11.8 bilioni
Mh Mgeni Rasmi
Kazi ya matengenezo ya jumba hili la treni ilianza
rasmi tarehe 2, Novemba 2016 baada ya mkandarasi kukabidhiwa jengo. Kazi za mwanzo
zilizofanyika ni kuliongezea umadhubuti jengo (strengthening of the building)
kwa kulihami lisije likaanguka au kuleta madhara kabla na wakati wa ujenzi.
Hatua iliyofuata ni kuliezeka jengo kwa kutumia
bati la Aluminium ambalo linastahamili upepo wa bahari tofauti na bati la
kawaida na hivyo kukaa muda mrefu bila ya kuharibika na kufanya kutu.
Katika hali inavyoonekana sasa kazi ya ukarabati wa
jengo ikiwa imekamilika ni pamoja na kuweka nguzo na bimu ili kuliongezea
umadhubuti jengo na kuweza kubeba uzito mkubwa zaidi, kazi ya kurekebisha kuta
zote, kutia plasta, kupaka rangi ndani
ya jengo, kufunga fremu mpya za milango na madirisha na kuweka dari
"ceiling".
Ukarabati wa jengo pia ulihusisha kazi za kumalizia
(finishing), ambapo kazi ya kutia rangi kuta za nje, kazi za kufunga
miundombinu ya maji na umeme, uwekaji wa madirisha na milango, ufungaji wa
ngazi, ujenzi wa mahodhi ya kuhifadhia maji safi, ujenzi wa mashimo ya maji machafu[k2] (septic tank) ufungaji wa lifti na kupanda miti ya
maua na majani katika eneo la bustani.
Mradi
huu awali ulitarajiwa kukamilika ndani ya kipindi cha miezi kumi na nane (18)
ilipofikia Mei 2018, ila badaa yake
uliongezwa muda wa miezi miwili na kukamilka mwishi wa mwezi Julai, 2018.
Mh Mgeni Rasmi
Mradi
huu wa kulifanyia matengenezo makubwa jumba la treni (Chawl Building) kwa
kuliongezea ubora na haiba ya jengo hili umebadilisha kwa kiasi matumizi,
ambapo Baada ya kukamilika kwake, jengo limekuwa na milango ya maduka 52,
sehemu 2 za ATM, sehemu ya kuswalia wanawake, nyumba 10 za kuishi (2 za vyumba
viwili na 8 za chumba kimoja) sehemu za ofisi, supermarket, sehemu ya kufanyia
mazoezi (Gymnasium) na mkahawa (restaurant).
Mradi
pia umezingatia uwepo wa watu wenye mahitaji maalum, hivyo umewekewa
"ramp" itayowawezesha kufika katika ghorofa ya chini na pia umewekewa
"lifti" ambayo itasaidia kuwafikisha katika ghorofa zilizobakia.
Mh.
Mgeni Rasmi
Naomba
ifahamike kwako kuwa Kampuni zote nilizozitaja zilipatikana kwa kuzingatia
taratibu na sheria za manunuzi za Zanzibar kwa maana zilishindanishwa na
kampuni nyingine kwa kuzingatia uzoefu, gharama na ubora wa kazi inayohitajika
kufanywa.
Mh.
Mgeni Rasmi
Uwekezaji
huu wa ukarabati wa jengo la treni ni mkubwa kwa ZSSF na kukamilika kwake
unaashiria kuanza kuingiza mapato, hivyo kutokana na uchambuzi uliofanywa na
wataalamu mbalimbali wakiwemo wa ZSSF, mradi huu utakuwa na tija kifedha,
kiuchumi na kijamii. Kwa kuzingatia vyanzo vya mapato vilivyomo, ZSSF
inatarajia mradi huu:
1. Utajilipa
ndani ya kipindi cha miaka kumi ijayo.
2. Aidha,
Serikali kupitia vyombo vyake vya kukusanya kodi itanufaika na biashara
zitakazoendeshwa na wananchi mbalimbali
katika jengo hili ambalo imezikosa kwa muda.
3. Taasisi
za Serikali kama Shirika la Umeme, Mamlaka ya maji wataweza kunufaika na mauzo
ya umeme na maji yenye kutumika katika
jumba hili.
4. Nadhani
pia mtakubaliana na mimi kuwa Haiba yake mpya itakuwa ni kivutio kikubwa kwa watalii
ambapo kila atayefika Unguja hatakosa kutembelea
hapa.
Mh.
Mgeni rasmi
Matengenezo
ya jumba hili ni miongoni mwa utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama cha
Mapinduzi ya mwaka 2015, ambayo ni kuwatengenezea makaazi mazuri kama haya, pia
kuwawekea mazingira mazuri ya kuendesha shughuli zao binafsi za kazi za
kujitafutia riziki halali. Tunaimani kuwa chini ya uongozi wako mahiri na
makini Rais wetu wa Zanzibar lakini pia ukiwa ni Makamo Mwenyekiti wa Chama
tawala Serikali yetu itapindukia yale yote yaliyopangwa katika ilani hiyo hadi
kufikia mwaka 2020.
Mh.
Mgeni rasmi
Naomba
nimalizie maelezo yangu mafupi kwa kukushukuru tena Mh. Rais kwa busara na maelekezo yako
yanayosaidia kutupa dira ya utekelezaji wa majukumu yetu. Mwisho napenda
kuwashukuru viongozi wangu kutoka Wizara ya Fedha, Mwenyekiti na Bodi ya
Wadhamini ya ZSSF, Menejimenti na
wafanyakazi wote wa ZSSF kwa mashirikiano na utendaji wa kupigiwa mfano.
Lakini
pia nimshukuru kwa kiasi kikubwa na kwa dhati kabisa Nd. Abdulwakil Haji Hafidh
Mkurugenzi Mwendeshaji aliyestaafu ambaye taasisi yetu hii kwa mafanikio
makubwa kabisa ikiwemo kuanzisha mradi huu.
“Wito
kwa wadau na wananchi wote kwa ujumla ni tulitunze jengo letu kwani waswahili
walisema kitunze kidumu”.
“Maendeleo ya Zanzibar yataletwa na
Wazanzibari wenyewe”
ZSSF
OYEEE
Ahsanteni
kwa kunisikiliza.
No comments:
Post a Comment