Na.Hussein
Makame, NEC
Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC)
imetangaza
Uchaguzi
Mdogo wa Udiwani
katika kata 21 za
mikoa 10 ya Tanzania
Bara
utakaofanyika
tarehe 16 Septemba mwaka huu.
Akitoa taarifa ya uchaguzi huo jijini Dar es
Salaam leo,
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Dkt.
Athumani
Kihamia, alisema fomu za uteuzi wa wagombea wa
uchaguzi huo zitatolewa kati ya
tarehe 17 hadi 23 Agosti
mwaka huu.
Aliongeza kuwa uteuzi wa wagombea utafanyika
tarehe 23
Agosti wakati kampeni za Uchaguzi zitafanyika kati ya tarehe
24
Agosti hadi tarehe 15 Septemba mwaka huu.
Dkt. Kihamia alisema kuwa Tume imetangaza
uchaguzi huo
baada ya kupokea taarifa ya uwepo nafasi wazi za udiwani
katika kata
hizo 21 zilizopo katika Halmashauri 15 kutoka
kwa Waziri mwenye dhamana na
Serikali za Mitaa.
“Nafasi wazi za udiwani katika Kata hizo
zimetokana na
sababu mbalimbali zikiwepo kifo, kujiuzulu, kutohudhuria
vikao na
kufutwa uanachama” alisema Dkt. Kihamia na
kuongeza kuwa;
“Baada ya kupokea taarifa hiyo na kwa
kuzingatia masharti
ya kifungu cha 13(3) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za
Mitaa; Tume ina utaarifu Umma kuhusu kuwepo kwa
Uchaguzi mdogo katika Kata hizo
21.”
Kufuatia taarifa hiyo, Dkt. Kihamia alitoa
mwaliko wa Tume
kwa vyama vya siasa, wadau wote wa Uchaguzi na wananchi kwa
ujumla kushiriki katika Uchaguzi huo.
“Tume inachukua fursa hii kuviasa vyama vya
siasa na
wadau wote wa Uchaguzi kuzingatia matakwa ya Katiba, Sheria ya
Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
(Madiwani) za mwaka 2015” alisema Dkt. Kihamia.
Aidha alivitaka vyama vya siasa na wadau wa
uchaguzi
kuzingatia Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na
Madiwani ya mwaka
2015 pamoja na maelekezo yote
yaliyotolewa au yatakayotolewa na Tume wakati wote
wa
Uchaguzi mdogo.
Uchaguzi huu mdogo wa udiwani katika kata 21
unatarajiwa
kufanyika sanjari na uchaguzi mdogo wa ubunge katika
majimbo ya
Korogwe Vijijini, Ukonga na Monduli na kata za
Tindabuligi na Kisesa katika
Halmashauri ya Wilayani
Meatu, uliotangazwa juzi ambao utakaofanyika siku ya
Jumapili tarehe 16 Septemba mwaka huu.
No comments:
Post a Comment