Habari za Punde

Watendaji Ofisi ya Rais Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na utawala bora watakiwa kufanya kazi kwa kushirikiana




RAYA HAMAD (ORKSUUUB)

Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria utumishi wa umma na Utawala Bora Mh Haroun Ali Suleiman amezitaka taasisi za kisheria zilizomo ndani ya Ofisi hio wakiwemo majaji , mahakimu na wanasheria kufanya kazi kwa mashirikiano ili jamii iweze kuelewa na kufahamu masuala ya sheria na kuwaepushia usumbufu wananchi .

Haroun amesema matatizo mengi ya kisheria  yanaweza kupunguwa kwa kufanyiwa kazi iwapo watendaji watakuwa na utaratibu wa kuwafuata wanajamii waliko kwa kuwapa elimu ikiwa ni pamoja na kutumia vyombo vya habari mbali mbali .

Aidha amewasiitiza viongozi wa Tume ya Kurekekebisha sheria  na Tume ya Utumishi wa Mahakama kulipa kipaubele suala la elimu kwa kusomesha watendaji wake pia kuendeleza uhusiano mwema wa kimataifa na nchi nyengine kwa lengo la kujenga uelewa zaidi na ushirikiano mwema kwa mataifa ya nje.

Nae Mwenyekiti wa Tume ya kurekebisha sheria Jaji Mshibe Ali Bakari ameitaka jamii kufatilia kwa karibu masuala ya sheria ili kuepusha migongano  isiyo ya lazima “hivi sasa tumeanza kuwafikia wanajamii waliko awali wananchi walikuwa na khofu ya kutoa maoni yao kuhusiana na sheria hii ilitokana na uwelewa mdogo waliokuwa nao ”alisisitiza Jaji Mshibe.

Akiwasilisha taarifa ya Tume hio Kaimu katibu ndugu Ali Juma Ali amesema kuwa Tume inawajibu wa kupendekeza mabadiliko ya sheria kwa mujibu wa mazingira ya Zanzibar ,kuhakikisha kuwa sheria zinatoa haki na usawa ,kutoa elimu kwa wananchi ili wapate uwelewa wa sheria zao ,kutafsiri sheria ili zifahamike kwa wanajamii, kushauri njia mpya za utekelezaji wa sheria, kuziweka pamoja sheria za Zanzibar, kuimarisha mashirikiano na taasisiza kimataifa zenye majukumu sawa na Tume  pia kuchapisha makala ya sheria za kimataifa ndani ya Zanzibar , ikiwa makala hayo yanakwenda sambamba na maadili ya mzanzibari.

Wakati huo huo Waziri Haroun ameitaka  Tume ya Utumishi Serikalini kuhakikisha inawahakiki waajiriwa kabla kuwaajiri jambo ambalo inatengeneza nidhamu ya kazi  uwajibikaji na maadili  ili kuwapata watumishi wenye nia na moyo wa kizalendo  kwa maslahi ya nchi

Haroun amesema Tume ndio inayojenga nidhamu na maadili Serikalini hivyo itakapochaguwa wajiiri wasio na uwezo na maadili ya kazi  itakuwa imekiuka misingi na taratibu za uajiri “inasikitisha kuona kuwa wafanyakazi wanafukuzwa kila mwaka kwa utovu wa nidhamu,kukosa uzalendo na sifa za kiutendaji  .

Amewaasa wajumbe hao kutojihusisha na masuala ya kupokea rushwa au kushutumiwa kwa kukiuka taratibu za kiuajiri kwa waombaji ambao hawatakuwa na sifa  na badala yake wakaingizwa kazini kwa upendeleo au rushwa hilo halitavumilika .

Nae Mwenyekiti wa Tume hio  Kombo Hassan Juma ameomba kupatikana  kwa ofisi ya  kufanyia kazi badala ya kutumia jengo waliopo hivi sasa la People Palace ambalo  mazingira yake hayako vizuri kiutendaji pia kulipa  umuhimu wa historia ya kipekee iliyopo katika Ofisi hizo ambazo hivi karibuni jengo hilo litafanyiwa marekebisho.

Katika risala iliyosomwa na Katibu wa Tume hio ndugu Mohammed Khamis amesema kuwa Tume  inamamlaka ya kuajiri watumishi wapya , kuthibitisha kazini watumishi , kuidhinisha nyongeza za muda wa utumishi , ajiira za mikataba , kupandisha daraja , kuidhinisha kustaafu kazi kwa watumishi waliofika umri wa kustaafu kazi kwa watumishi waliofikia umri wa kustaafu kazi kwa lazima , kustaafu kwa maradhi na kustaafu kwa hiari, kubadilisha kada na kuacha kazi.

Aidha Tume ina wajibu wa kusimamia haki na nidhamu za watumishi walio chini ya usimamizi wa tume ikiwa ni pamoja na kuidhinisha kufukuzwa kazi watumishi waliokwenda kinyume na sheria, kanuni na taratibu za utumishi , kupokea  kusikiliza na kuyatolea maamuzi sahihi malalamiko na rufaa zote zinazowasilishwa baada ya kuzingatiwa taratibu zote kwa mujibu wa sheria  na kanuni .

Akielezea mafanikio ya Tume hio Bw Mohammed amesema katika mwaka 2017/ 2018  Tume imeajiri vijana 2968 kwa Unguja na Pemba kati yao 2023 walikuwa ni wanawake sawa na asilimia 68.2 na wanaume 945 sawa na asilimia 31.8 ambapo kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2017/2018 Tume  ilipokea jumla ya maombi ya kazi 29774 ambapo pia Tume imeidhinisha kufukuzwa kwa kazi watumishi 129 kutokana na makosa mbali mbali ya utovu wanidhamu hasa utoro kazini

 Nae Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Katiba Sheria utumishi wa umma na Utawala Bora Nd Yakout Hassan Yakout amesema lengo la ziara hio ni kuangalia mazingira ya kazi na fursa za watendaji , changamoto na mafanikio

Wafanyakazi wa Tume hio wameahidi kuendelea kufanya kazi kwa uadilifu pamoja na mazingira magumu waliyonayo

Mhe Haroun ameizindua Tume ya Utumishi Serikalini ambapo imeanzishwa  kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ibara ya 117 toleo la mwaka 2016 sambamba na kifungu 33cha sheria ya sheria Utumishi wa Umma No. 2 ya mwaka 2011 .







No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.