Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi wa Umma na Utawala Bora Zanzibar Mhe. Haroun Ali Suleiman akizungumza na Uongozi na Wafanyakazi wa Tume ya Maadili ya Viongozi Zanzibar wakati wa ziara yake kutembelea Idara zilioko katika Wizara yake. akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo na Watendaji wa Tume hiyo.
Na. Raya Hamad (OR.KSUUUB)
Watendaji
wa Tume ya maadili ya viongozi wa Umma wametakiwa kuendeleza uaminifu wenye nidhamu na uadilifu katika kutekeleza
majukumu ya kazi zao kama Serikali ilivyowaamini kuwakabidhi majukumu hayo.
Hayo
yameelezwa na Waziri wanchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi wa Umma na Utawala
bora Mheshimiwa Haroun Ali Suleiman wakati alipofanya mazungumzo na viongozi
pamoja na watendaji wa Tume ya maadili ya viongozi wa Umma Waziri
Haroun amesema nchi haiwezi kuwa na Taifa lenye heshima na nidhaamu bila kuwepo
na maadili hivyo utunzaji wa siri ni muhimu hasa kwa chombo kinachoaminiwa kama Tume ya maadili ya viongozi wa Umma “ haitapendeza kuona siri za viongozi wa serikali zinatoka nje ama kusambaa kinyume
na utaratibu ”alisisitiza Haroun.
Aidha
Haroun amesisitiza kuwa mjenga nchi ni mwananchi hivyo amewataka
watendaji hao kuwa na ari na bidii ya kujituma ili kufikia malengo
waliyojipangia wakiamini kuwa hakuna atakaekuja kujenga Taifa lao bila
ya kuanza wao wazalendo na wengine hufuatia .
Nae
Katibu wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma Ndugu Kubingwa Mashaka Simba amesema Tume inajukumu la kupokea ,
kusajili na kuhakiki tamko la mali na madeni kutoka kwa viongozi wa Umma ,
kupokea malalamiko na kufanya uchunguzi wa tuhuma za uvunjaji wa Sheria ya
maadili ya Viongozi wa umma na kutoa elimu kwa umma na viongozi kuhusu umuhimu
wa kuimarisha maadili Kutoa ushauri, maelekezo na miongozo kuhusiana
na maadili ya viongozi wa umma ikiwa ni pamoja na kuhakiki taarifa za mali
na madeni ya viongozi wa umma
Hata hivyo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2017/2018 imepokea na kusajili jumla ya fomu za taarifa za mali na madeni za viongozi wa umma 1,631 sawa na asilimia 99 ya shabaha iliyopangwa ya kupokea fomu za tamko la mali na madeni.
Hata hivyo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2017/2018 imepokea na kusajili jumla ya fomu za taarifa za mali na madeni za viongozi wa umma 1,631 sawa na asilimia 99 ya shabaha iliyopangwa ya kupokea fomu za tamko la mali na madeni.
Kubingwa
amesema kuwa Tume inaendelea kutoa elimu kwa viongozi ili kujiepusha na matendo
ya ukiukwaji wa maadili na kuwakumbusha viongozi wa umma juu ya umuhimu wa kukuza maadili na kuongeza kasi ya kuwatumikia wananchi ili kufikia malengo ya
kitaifa na umuhimu wa kuimarisha maadili.
Jumla
ya mikutano 37 iliyowashirikisha viongozi wa umma kutoka Taasisi mbalimbali za
Serikali na kamati za masheha imefanyika Unguja na Pemba , mikutano na mabaraza
ya vijana katika Mkoa wa Mjini Magharibi uliowashirikisha viongozi wa mabaraza
150 ili kukuza uelewa wa vijana ili kukuza uwelewa wa vijana juu ya majukumu ya
Tume na
kuwaandaa vijana hao kimaadili ili wawe viongozi wazuri wa baadae.
kuwaandaa vijana hao kimaadili ili wawe viongozi wazuri wa baadae.
Katika
kukabiliana na baadhi ya changamoto Tume imeendelea na jitihada ya kuishajihisha jamii ili kuwa na uwelewa wa kutosha kuhusu Tume ya Maadili ya
Viongozi wa Umma kwani bado wapo baadhi
ya wanajamii hawajawa na uelewa wa kutosha kuhusu majukumu yake, aidha Tume
inaendelea kushirikiana na Idara ya Serikali mtandao ili kupata mfumo imara na
salama wa elektronik utakaoweza kutunza taarifa hizo.
Tume
ya maadili ya Viongozi wa Umma imeanzishwa chini ya sheria ya maadili ya
Viongozi wa Umma, Nambari 4 ya mwaka 2015 na kuanza kazi rasmi mwezi April 2016
No comments:
Post a Comment