Habari za Punde



Baada ya kumalizika ligi kuu soka ya Zanzibar na kupatikana kwa Bingwa wa ligi hiyo ambae ni JKU pamoja na Zimamoto ambae ni Makamo Bingwa, sasa Kamati inayosimamia Mashindano hayo imejipanga kumaliza vyema kwa upande wa Kombe la FA ambalo bado linaendelea sasa.

Akizungumzia nasi Katibu wa Kamati ya Mashindano hayo Alawi Haidar Foum amesema baada ya kumaliza ligi kuu na ligi ya Mabingwa wa Wilaya sasa wamejipanga imara kulimaliza Kombe la FA.

Msimu mpya wa mwaka 2018-2019 unatarajiwa kuanza rasmi siku ya Alhamis ya Oktoba 18, 2018 saa 10:00 za jioni katika Uwanja wa Amaan, kwa kuchezwa mchezo wa Ngao ya Jamii ambao utawakutanisha   Bingwa wa ligi kuu (JKU) na Bingwa wa Kombe la FA (Bado hajajulikana).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.