Mbunge
wa jimbo la Vwawa ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.
Japhet Hasunga akikabidhi seti ya jezi kwa Mwalimu wa michezo Simoni Kalinga wa Shule ya Sekondari ya Isandula iliyopo
wilaya ya Mbozi mkoani Songwe.
Mbunge
wa jimbo la Vwawa ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.
Japhet Hasunga akipeana mkono wa shukrani kutoka Mwalimu wa michezo, Aloyce Mwambungu
wa Shule ya Sekondari ya Msankwi iliyopo wilaya ya Mbozi mkoani Songwe
Mwanakijiji
wa Kijiji cha Mafumbo, Richard Allen akikabidhiwa mpira kwa ajili ya timu ya
kijiji hicho wakati Mbunge wa jimbo la Vwawa ambaye pia ni Naibu Waziri wa
Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga alipowatembelea kwa ajili ya
kuzungumza nao.
Mbunge
wa Jimbo la Vwawa amabaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.
Japhet Hasunga akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Isalalo iliyopo wilaya ya Mbozi mkoani Songwe mara
baada ya kuwakabidhi vifaa vya michezo.
1. Baadhi
ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Msankwi iliyopo wilayani Mbozi mkoani Songwe
wakimsikiliza Mbunge wa jimbo la Vwawa ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili
na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga wakati alipowatembelea kwa ajili ya kuwakabidhi
vaifaa vya michezo.
Na.lusungu helela
MBUNGE wa Jimbo la Vwawa ambaye pia ni Naibu Waziri wa
Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet
Hasunga amekabidhi seti za jezi
pamoja na mipira yenye zaidi ya thamani ya sh.milioni 17 katika shule za Sekondari za kata nne zilizopo katika jimbo hilo.
Mbali ya kugawa vifaa hivyo, Mhe. Japhet Hasunga ametoa
zawadi kwa baadhi ya wanafunzi waliofanya vizuri katika masomo ya Hesabu,
Fizikia pamoja na masomo mengine katika mitihani ya taifa kwa kidato cha pili na cha nne ikiwa ni
utekelezaji wa ahadi alizokuwa ameahidi kwa wanafunzi hao
Akikabidhi vifaa kwa nyakati tofauti wilayani Mbozi mkoani
Songwe katika shule hizo, Mhe. Hasunga amesema ameamua kutoa vifaa hivyokwa lengo la kusaidia Serikali katika juhudi za
kuinua michezo lakini pia ni sehemu ya kazi zake kama Mbunge
Ameongeza kuwa
michezo licha ya kujenga utimamu wa mwili lakini pia ni ajira huku akitoa mfano
kuwa kati ya watu wanaolipwa mishahara mikubwa duniani wachezaji ndio
wanaoongoza.
Pia amesema kuwa anatambua kuwa kuna changamoto za kutosha
katika michezo hususani vifaa vya michezo Kwa kutambua hilo ameamua kutoa vifaa
hivyo huku akiwataka wanafunzi na walimu hao kusimamia vyema
Katika hatua nyingine, Mhe. Hasunga amewataka walimu pamoja
na wanafunzi kujenga utamaduni wa kutembelea vivutio vya utalii kwa ajili ya
kupumzika na pia ni fursa ya kuweza kujifunza vitu vipya tofauti na vile
walivyovizoea.
No comments:
Post a Comment