Habari za Punde

Mradi wa Best Of Zanzibar Yakabidhi Kituo Cha Watu Wenye Ulemavu wa Jimbo la Shaurimoyo Zanzibar.


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Mkurungenzi Mkuu wa Kampuni ya Pennyroyal Ltd Bw. Brian Thomson, alipowasili katika viwanja vya Kituo cha Watu Wenye Ulemavu wa Jimbo la Shaurimoyo kilichojengwa na Kampuni yake kupitia Mradi wa Best of Zanzibar, wakati wa hafla hiyo ya ufunguzi na kukabidhi Kituo hicho Kwa Wananchi wa Jimbo hilo.baada ya kuweka jiwe la msingi, kulia Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud. 
Makamu wa Pili wa Rais wa Zazibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na kumkabidhi Baskeli mmoja wa Mwananchi Mwenye Ulemavu wa Jimbo la Shaurimoyo baskeli zilizotolewa na Mradi wa Best of Zanzibar, ya Kampuni ya Pennroyal inayojenga Kijiji cha Kitalii Matemwe Zanzibar.hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Kituo hicho baada ya ufunguzi wake.


Na.Mwandishi Wetu.
Katika juhudi za kuendeleza kuboresha maisha ya Wazanzibari, Blue Amber kupitia kitengo chake cha kusaidia jamii Best of Zanzibar kimeungana na Viongozi wa Chama Cha Walemavu kwa kujenga kituo cha Watu wenye UlemavuShaurimoyo.

Katika jimbo la Shaurimoyo kuna baadhi ya wananchi walemavu wanaojishughulisha na miradi tofauti ya biashara ili kujipatia kipato na kuwasaidia katika mahitaji yao ya kila siku. Viongozi wa chama cha walemavu na Mhe. Hamza Juma walitaka kuboresha mazingira  wanayofanyia biashara, 

hivyo walikutana na Mkurungenzi Mkuu wa Kampuni ya Pennyroyal Ltd Bw. Brian Thomson na kumwelezea mahitaji ya Walemavu katika jimbo la Shaurimoyo. Bw. Brian Thomson hakusita na kukubali kujenga kituo hicho cha walemavu ili kusaidia wanajamii hao. Kituo hicho kitawezesha vijana na wazee kupata mafunzo mbali mbali na kuwawezesha walemavu hao kufanya biashara zao.

“Napenda kuleta mabadiliko chanya duniani, japo hata kwa mtu Mmoja. Naamini unapo msaidia mtu Mmoja anaweza saidipia familia na jamii inayo mzunguka. Kwa sababu hii, Pennyroyal Ltd inafanya kazi kwa karibu na jamii ya waleavu ili kuleta mabadiliko kwa watoto, wanaume na wanawake wasiojiweza.” Alisema Bw. Brian Thomson Mkurungenzi 

Mkuu wa Pennyroyal Ltd. “Nataka kuweka msisitizo kwa sekta binafsi na wawekezaji waliopo Zanzibar kuungana nasi nakujenga vituo kama hivi katika majimbo mengine na kuwafikia wananchi wengi zaidi Zanzibar.” Aliongezea Bw.Thomson.

Meneja wa programu ya Best of Zanzibar Bi. Aminata Keita alisema “Kama Kampuni tunaamini kwamba tukiandaa mazingira mazuri ya kufanya kazi na kusaidia watu wasiojiweza tunawapa nafasi nzuri ya kujiendeleza na kujifunza biashara mbali mbali zitakazo wawezesha kupata ajira na kujikwamua kiuchumi. Hivyo basi naomba viongozi na wanajamii wote watunze kituo hichi ili kusaidia kizazi kijacho na kuleta maendeleo endelevu. Juhudi zetu kwa pamoja zitasaidia kuwafikia wengi wasiojiweza katika jamii, tunataka mradi huu uguse maisha ya watoto na watu wazima,ndio mana tunahitaji kila mmoja aupe uzito ili ufanikiwe.

Nae Mwakilishi wa jimbo hilo Bwana Hamza Hassan Juma, alitoa wito kwa Wawekezaji wengine na wasamaria wema kuunga mkono juhudi za Best of Zanzibar. “Tunaishukuru Best of Zanzibar kwa msaada huu na tunaishukuru Pennyroyal Ltd kama Mwekezaji kwa jitihada zao kubwa katika kuboresha maisha ya wasiojiweza. Kuna wengi wanaohitaji katika jimbo letu ambao kwa Pennyroyal na Serikali peke yao hawawezi kuwamaliza, tunahitaji wadau wengine kuungana nao katika juhudi hizi za kuboresha maisha kwa wasiojiweza.”

Kituo hicho kilifunguliwa rasmi na Makamo wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi. Balozi Seif aliwapongeza Pennyroyal kwa kazi nzuri wanayofanya na kuwa mfano wa kuigwa na Wawekezaji wengine. “ Tunashukuru sana msaada kutoka Best of Zanzibar na mchango wao mkubwa kwenye elimu na kuwawezesha wanajamii.” Alimalizia Balozi Seif Pamoja na ufunguzi wa jengo hilo, Mr. Brian Thomson amewalipia Bima ya Afya watoto 50 walemavu na kuchangia Milioni moja taslim kwenye Account ya Manedeleo ya Walemavu. Kwa kuongezea, Best of Zanzibar imetoa baskeli nne za walemavu, vifaa vya ofisini kama kompyuta, printa, mashine ya fotokopi, lamineshen na nyenginezo ili kurahisisha kuendeleza vizuri ofisi hiyo.

Kwa maelezo zaidi kuhusu Best of Zanzibar unaweza 
kututembelea kupitia: www.best-of-zanzibar.com na Blue Amber Zanzibar unaweza kutembelea: www.blueamberzanzibar.com

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.