Habari za Punde

Naibu Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Aongoza Harambe ya Kuchangia Fedha Kwa Ajili ya Maendeleo ya Chuo Cha ST. Mark's Jijini Dae es Salaam.

Naibu Spika wa Bunge Mh. Dkt. Tulia Ackson akimwakilisha Spika wa Bunge Mh. Job Ndungai aliongoza Harambee ya changizo la fedha kwa ajili ya maendeleo  chuo cha St. Mark’s ambacho kipo Buguruni Malapa Jijini Dar es Salaam.

Katika harambee hiyo Dkt. Tulia aliwezesha kuchangisha Tsh Milioni 284 kwa umahili mkubwa ambapo alitumia njia mbalimbali pamoja na  mistari  ya Bibilia ambayo iliwahamasisha watu wengi kuchangia jambo ambalo wengi hawakutarajia.

Katika harambee hiyo pamoja na waumini na wageni mbalimbali kuhamasishwa kuchangia fedha hizo  na  Dkt. Tulia, lakini pia bila woga aliwabana Maaskofu, wachungaji na wainjilisti ili wapate kuchangia katika harambee  hiyo.

Naibu Spika wa Bunge Mh. Dkt Tulia Ackson akizindua rasmi harambee ya kuchangia maendeleo ya chuo cha St. Mark's ambapo alisema kuwa yeye hato ongea mengi zaidi ya kukusanya fedha kwa kuwa jambo hilo ni muhimu.
 Baba Askofu Afidh abeid (aliyeshika kipaza sauti) akiomba kwa ajili ya ufunguzi wa Harambee ya kuchangia fedha za maboresho chuo hicho
Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Dkt. Maimbo Mdolwa akitoa neno la Shukurani kwa Mgeni rasmi Naibu Spika wa Bunge Mh. Dkt Tulia Ackson  kwa kukubali kuungana nao katika harambee ya kuchangia fedha  kwa ajili ya maendeleo ya chuo hicho.
Kaimu Mkuu wa Chuo cha St. John Prof. Emmanuel Mbennah akizungumzia kuhusu maudhui na nia ya kufanya harambee ya kupata fedha kwa ajili ya maendeleo  ya chuo cha St. Mark's
Mwenyekiti wa Kamati ya kuchangisha fedha za maboresho ya Chuo cha ST. Mark's Jaji Mkuu Mstaafu Mh. Agustino Ramadhani akielezea historia ya chuo cha St. Mark's tangia kilipo anzia hadi sasa.
Mgeni rasmi  Naibu Spika wa Bunge Mh. Dkt Tulia Ackson(Kushoto) akipokea zawadi kutoka chuo cha St. Mark's
 Mgeni Rasmi Naibu Spika wa Bunge Mh. Dkt Tulia Ackson pamoja na Meza kuu wakitoa mkono wa salam wakati waumini na wageni waalikwa walipokuwa wakitoa sadaka.
Kaimu Mkurugenzi wa Chuo cha St. Mark's Dkt. Peter Kopweh akizungumza jambo wakati wa Harambee ya kuchangiza fedha za Maboresho ya chuo hicho.
Mh. Balozi Lupia akizungumza jambo wakati wa Harambee ya kuchangia maendeleo ya chuo hicho
Baadhi ya watu wakitoa ahadi pamoja na michango yao
Sr. akitoa neno pamoja na maombi wakati wa harambee ya kuchangisha  fedha kwa ajili maboresho ya chuo hicho.
Mgeni Rasmi Naibu Spika wa Bunge Mh. Dkt Tulia Ackson akionesha picha ambayo allichorwa na mmoja muumini wa Kanisa la Anglikana.
Mgeni Rasmi Naibu Spika wa Bunge  Mh. Dkt Tulia Ackson, akipokea kwa niaba picha ya Spika wa Bunge Mh. Job Ndungai.
Baadhi ya Wachungaji pamoja na watumishi wengine ambao wanasomea Uchungaji wakiwa katika Harambee hiyo.
Waumini, Waalikwa  mbalimbali pamoja na watumishi wa Chuo cha St. Mark's wakiwa katika Harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya maboresho ya Chuo hicho.
Kwa ambao wangependa kuchangia wanaweza kutumia njia zifuatazo
TIGO PESA : 0677058716

CRDB BANK: 0150237155300 (HOLLAND BRANCH)

TIB : 004600000860601 (SAMORA DAR ES SALAAM)

(Picha zote na Fredy Njeje)




No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.