Mkurugenzi wa Taasisi inayojishughulisha na masuala ya usalama barabarani ,Pily Hamisi Layda (kushoto) akimkabidhi Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti wa
Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni, mpango kazi wa Kampeni Maalumu ya Usalama Barabarani na Udhibiti wa Ajali iliyozinduliwa katika Uwanja wa Skuli ya Jang’ombe, leo Visiwani Zanzibar
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti wa
Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni, akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa
Shule ya Msingi Jang’ombe, Tiffy Mustafa (kushoto), moja ya kikoti maalumu
watakachokua wanavaa wanafunzi watakaoteuliwa kuwasaidia wenzao kuvuka barabara baada ya kuzindua Kampeni Maalumu ya Usalama Barabarani na Udhibiti
wa Ajali katika Uwanja wa Skuli ya Jang’ombe, leo
Visiwani Zanzibar.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti wa
Baraza la Taifa la Usalama Barabarani,
Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza wakati ya Uzinduzi wa Kampeni Maalumu ya Usalama Barabarani na Udhibiti wa Ajali
katika Uwanja wa Skuli ya Jang’ombe, leo Visiwani Zanzibar.
Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Jang’ombe, Aisha Abdallah Haji, akiuliza swali
linalohusiana na uvukaji wa barabara kwa watu wenye ulemavu wakati wa Uzinduzi
wa Kampeni Maalumu ya Usalama Barabarani na Udhibiti wa Ajali
katika Uwanja wa Skuli ya
Jang’ombe, iliyozinduliwa leo Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani,
Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani), Visiwani Zanzibar
Wanafunzi
wakifurahia jambo wakati Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti wa
Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani),
akizungumza baada ya kuzindua Kampeni Maalumu ya Usalama Barabarani na Udhibiti wa Ajali katika Uwanja wa Skuli ya Jang’ombe, leo Visiwani Zanzibar.
Picha na Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
Naibu Waziri wa Mambo
ya Ndani ya Nchi, ambae pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama
Barabarani, Mhandisi Hamad Masauni, amewatadharisha wamiliki wa shule zinazotumia magari mabovu kubebea wanafunzi
ikiwa ni kinyume na sheria za usalama barabarani hali ambayo inaweza kupelekea
ajali.
Akizungumza wakati wa
Uzinduzi wa Kampeni Maalumu ya Usalama
Barabarani na Udhibiti wa Ajali katika Uwanja wa Skuli ya Jang’ombe, Naibu
Waziri Masauni aliwataka wamiliki wa shule kuhakikisha wanatumia mabasi imara ili
kuepusha ajali na kuwaasa madereva wa magari hayo kufuata sheria za barabarani
“Wamiliki wa shule
wanatakiwa wafuate sheria kwa kuacha
kutumia mabasi mabovu na kujaza
wanafunzi kupita kiasi na tutatumia kikosi cha usalama barabarani kuhakikisha
wanafunzi wanakua salama muda wote wakiwa wanaenda shule na kurudi nyumbani.
“Nawaagiza askari wa
usalama barabarani kusimamia sheria ili wamiliki watakaokiuka sharia hizo waweze
kuchukuliwa hatua pamoja na madereva watakaobainika kuendesha magari mabovu
ambayo ni hatarishi kwa wanafunzi,” alisema Masauni
Akitoa ripoti ya
matukio ya ajali za barabarani Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi Zanzibar,
Shukuru Amir Ally alisema jumla ya ajali 229 zimeripotiwa ndani ya mwaka huu
tofauti na mwaka 2017 ambapo jumla ya ajali 391 zikiripotiwa huku akitoa siri
ya kupungua kwa ajali hizo ni ushirikiano wanaoupata kutoka kwa wadau wa
usalama barabarani.
Akisoma risala ya
uzinduzi huo Mkurugenzi wa Taasisi inayojishughulisha na masuala ya usalama
barabarani ya New Vision, Pily Hamis Ladya alisema wamedhamiria kufikia mikoa
yote ya Zanzibar na katika awamu hii ya kwanza wanaanza na shule kumi huku
akiahidi kuzifikia shule zote katika kutoa elimu ya usalama barabarani kwa
wanafunzi.
“Tunategemea kutoa
elimu hii ya usalama barabarani ili kuweza kuwaepusha na kuwalinda wanafunzi
wetu na majanga ya barabarani ili waweze kwenda shule na kurudi nyumbani
salama,” alisema.
No comments:
Post a Comment