Habari za Punde

MAONYESHO YA KIMATAIFA YAFUNGULIWA NA BALOZI MAHIGA JIJINI ARUSHA

Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika mashariki Balozi Agustine Mahiga akitoa hotuba kabla ya kuyafungua maonyesho hayo ya siku moja mwishoni mwa wiki jijini arusha

Na Ahmed Mahmoud Arusha
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Kikanda, Dk, Agustine Mahige amesema kuwa Tanzania haijamfukuza balozi wa Umoja wa Ulaya Nchini Tanzania, Reoland van de Geer bali ameitwa nyumbani na Umoja wa nchi hizo kw mshauriano. 
Aidha amepongeza mashirika ya Kimataifa yaliyopo nchini kwa kuandaa siku maalum ya kuwaonyesha wananchi fursa na kazi wanayofanya katika kukuza uchumi ikiwemo kuhakikisha muuaji ya kimbari yaliyotokea nchini Rwanda hayajirudii tena. 
Akizungumza Leo Novemba 3, Jijini Arusha katika maonyesho ya mashirika ya kitaifa yenye makao makuu yake Jijini Arusha  Dk, Mahige alisema kuwa ni jambo la kawaida kwa mabalozi wanaowakilisha nchi zao kuitwa na nchi zao kwaajili ya kupewa majukumu mengine au kutoa tathimini ya masuala waliyoyafanya. 
Dk, Mahige alisema uwepo wa Mahakama inayoshugulikia muuaji ya kimbari (MICT) ni kuhakikisha muuaji ya kimbari hayatokei tena katika nchi za Afrika na kutoa rai kwa mashirika ya Kimataifa yaliyopo nchini kutunza kumbukumbu muhimu ikiwemo za muuaji ya kimbari. 
Alisema maneno au vitendo yanayotolewa na wananchi katika nchi mbalimbali yanatakiwa kupingwa kwa nguvu zote kwani yanaweza kuibua hisia na kupeleka muuaji au kuleta chuki baina ya watu na watu au hata kupeleka mauaji. 
Alisisitiza kuwa ni vyema sasa mahakama hiyo ikawajengea uwezo wanazuoni wa masuala ya kisheria kwa Tanzania na nchi za Afrika ikiwemo kuzingatia utawala wa sheria na demokrasia pamoja na haki za binadamu. 
Awali Mkuu wa shughuli za Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Alvaro Rodriguez alisema kuwa Tanzania inajitahidi kukahakikisha malengo endelevu yanazingatiwa ikiwemo kuhakikisha maendeleo yanapatikana kwa kila mtanzania. 
Naye Afisa Mwandamizi wa Utafiti kutoka Taasisi ya  Sheria za Kimataifa, Profesa Mathias Sahinkuye alisema masuala ya sheria  ni muhimu ili kuhakikisha nchi zinakuwa na amani 
Awali Meya wa Jiji la Arusha Kalist Lazaro,ambaye ndiye mwasisi wa Maonyesho hayo amesema tangu kuanza kwa Maonyesho hayo mwaka Jana kumekuwa na mafanikio makubwa kwa jamii kujifunza fursa mbalimbali za Kimataifa.
"Mjumuiko wa wananchi katika Maonyesho hayo ya Kimataifay umekuwa na manufaa makubwa kwani kumekuwepo na mabadiliko na mafanikio makubwa kwa wananchi kujifunza na kujionea fursa za kibiashara" Amesema Meya.

Waziri wa Mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa Afrika mashariki Balozi Agastine Mahiga alipukokuwa akifungua maonyesho ya mashirika ya kimataifa yanayofanyakazi jijini Arusha mwishoni mwa wiki kwenye mahakama ya kimataifa ya MICT ilyopo eneo la laki laki nje kidogo ya jiji la Arusha
Sehemu ya viongozi mbali mbali wa mashirika ya kimataifa yanaofanyakazi jijini hapa akiwamo Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika mashariki Balozi Agustine Mahiga na meya wa jiji la Arusha Kalist Lazaro pamoja na Naibu meya wa jiji hilo mwenye miwani nyeusi Paul Mattsen wakifuatilia ufunguzi wa maonyesho ya kimataifa ya mashirikia ya kimataifa yanayofanyakazi jijini Arusha
Sehemu ya viongozi mbali mbali wa mashirika ya kimataifa yanaofanyakazi jijini hapa akiwamo Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika mashariki Balozi Agustine Mahiga na meya wa jiji la Arusha Kalist Lazaro pamoja na Naibu meya wa jiji hilo mwenye miwani nyeusi Paul Mattsen wakifuatilia ufunguzi wa maonyesho ya kimataifa ya mashirikia ya kimataifa yanayofanyakazi jijini Arusha
Mstahiki Meya wa jiji la Arusha Kalist Lazaro akitoa hotuba yake wakati waa ufunguzi wa maonyesho ya kimataifa ya mashirika kimataifa yanayofanya kazi jijini Arusha yaliofunguliwa na waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Balozi Agustine Mahiga jumamosi iliyopita jijjini arusha picha na mahmoud ahmad arusha
Sehemu ya mabanda ya mashirika ya kimataifa yalioshiriki maonyesho hayo kwenye viwanja vya mahakama ya kimataifa ya kimbari (MICT) eneo la Laki laki nje kidogo ya jiji la Arusha picha na mahmoud ahmad arusha

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.