Mwandishi
wetu-MAELEZO.25-1-2019.
SERIKALI itaendelea
kushirikiana na sekta binafsi katika kutoa fursa kwa watu wengi kwa kuwezesha
utekelezaji wa miradi mingi kwa mapana, katika Taasisi za serikali na Taasisi
binafsi.
Akizungumza katika
mjadala wa Clouds Media katika kipindi cha The
Big Breakfast chenye kauli mbiu ya The
power of Man yaani Nguvu ya Pamoja kilichofanyika leo Jijini Dar es Salaam katika
hoteli ya Serena, Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa
Serikali Dkt Hassan Abbasi alisema kuwa serikali inaendelea na jukumu la ujenzi
wa nchi kwa kushirikiana na sekta binafsi.
“Tunatambua na
kuheshimu nguvu ya wengi kama kauli mbiu hii inavyoeleza, katika dhana ya
maendeleo kuna mengi Serikali inafanya ili kutekeleza azma yake kwa wananchi,
mfano Ujenzi wa madaraja mbalimbali nchini, Miradi ya Maji, Miradi ya Umeme,
Ujenzi wa vituo vya afya na Hospitali na kulete ndege, kwetu sisi haya ni
maendeleo makubwa sana”, Dkt. Abbasi.
Katika dhana ya Nguvu
ya pamoja, Dkt. Abbasi alisema kuwa kauli mbiu hii inaonesha namna gani sasa
haya mambo ambayo Serikali inafanya yanawafikia wananchi na kuwanufaisha popote walipo.
Dkt.Abbasi alieleza
kuwa katika mjadala wa nguvu ya pamoja
dhana ya maendeleo ina nadharia mbili ambazo wasomi wanazijadili
duniani kote ikiwa ni moja ya miongozo ya maenedeleo duniani, huku wakiamini
katika nadharia ya maendeleo ni watu na
wengine wakiamini katika nadharia ya maendelo ni vitu.
“nilichokisema ni kwamba
duniani kuna mjadala mkubwa sana katika suala la maendeleo, wapo wanaoamini kwamba maendeleo ni
watu kwa mambo yanafanyika moja kwa moja na yanagusa watu, wapo wanaoamini kwamba
maendeleo ni vitu kwamba huwezi kuwaendeleza watu bila kuwajengea miundombinu
kama vile barabara, reli, umeme na maji”, Dkt Abbasi.
Katika kuunga mkono
kauli mbiu ya nguvu ya pamoja, Dkt Abbasi alieleza kuwa katika nadharia mbili
za maendeleo Serikali inaamini katika nadharia zote yaani maendeleo ni vitu kwani inatekeleza miradi
mbalimbali kama barabara, Umeme, Maji, Afya na elimu, huku ikiwawezesha
wananchi kupata elimu bure, dawa katika vituo vya afya na umeme, ambao kwa sasa
unafika mpaka vijijini kwa maana ya maendeleo ni watu.
Aidha Dkt Abbasi
alieleza kuwa kauli mbiu ya Nguvu ya pamoja kutoka Clouds Media ni moja ya njia
kubwa katika kutimiza malengo la wananchi kwa kutekeleza na kusimamia miradi
mbalimbali ambayo ndiyo inawawezesha
wananchi kufanya shughuli zao za maendeleo.
Kwa upande wa sekta
ya habari Dkt.Abbasi alieleza kuwa Serikali inafanya kazi kubwa kwa
kushirikiana na sekta binafsi katika sekta hiyo muhimu pamoja na sekta zingine
ambazo zinawezesha wananchi kujikwamua kimaendeleo.
“Serikali ndiyo
mwezeshaji mkuu wa sekta mbalimbali, Sekta haiwezi kufanya kazi nchini bila Serikali
kuiwezesha kwa hiyo katika dhana hiyo hiyo ya Nguvu ya pamoja Serikali
inashiriki kwa nguvu zote”, Dkt Abbasi.
Dkt. Abbasi aliongeza
kuwa Serikali itaendelea kuheshimu uwepo wa sekta binafsi katika sekta ya
habari kwani mpaka sasa imewezesha upatikanaji wa leseni kwenye majarida na
mageti 202, Vituo vya Televisheni 35 na Redio 160.
Alieleza pia kuwa
nguvu ya pamoja ni pamoja na watendaji wa Serikali kushirikiana na sekta
binafsi ili kuwawezesha kupata huduma
mara moja pale inapohitajika kwa sababu watakuwa wanatenda jambo la
kuwafanya wengi kupata ajira katika sekta hizo.
“Ukiangalia
uanzishwaji wa viwanda ni lazima kuna mtendaji alijituma kutoa leseni,
maendeleo ya biashara mbalimbali, kilimo na sekta zingine ni lazima upate
leseni ni hata kwenye sekta ya habari
hii inamaana kuwa mtendaji wa Serikali unapoharakisha kwa kufuata sheria na
taratibu kuhakikisha mtu anapata leseni ya kuanzisha kiwanda, Biashara kubwa au
gazeti utakuwa umeajiri watu wengi bila kujua na hii ndiyo the power of man (Nguvu ya pamoja)”, Alisisitiza Dkt. Abbasi.
Kwa upande wake
Mkurugenzi Mkuu na Mumiliki wa Clouds media Group Joseph Kusaga aliahidi
kushirikiana na Serikali katika kutangaza maendeleo ya nchi hasa kwenye sekta
ya usafiri wa anga (shirika la ndege la Tanzania AirTanzania) pamoja na sekta
ya utalii katika kampeni mbalimbali
zitakazokuwa zinatangazwa Clouds Media.
No comments:
Post a Comment