Habari za Punde

Serikali Kuhifadhi na Kutangaza Historia ya Utamaduni wa Chifu Kingalu

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mheshimiwa Dkt.Harrison Mwakyembe akitoa maelekezo kwa  Idara ya Utamaduni kufika katika himaya ya Chifu Kingalu kwa ajili ya kukusanya taarifa muhimu za utamaduni usiyoshikika zenye historia ya zaidi ya miaka mia nne kwa ajili ya kuhifadhi na kutangaza kwa mashirika ya kimataifa  leo katika kijiji cha Kinole Mkoani Morogoro katika hafla ya makabidhiano ya zana za kijadi za Chifu Kingalu Mwanabanzi wa Kwanza zilizokuwazimeibiwa na kurudishwa katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro .
Chifu Kingalu Mwanabanzi XV (wa kumi) akizungumza wakati wa sherehe za makabidhiano ya zana za jadi za chifu huyo wa kwanza zilizokuwa zimeibiwa tangu kipindi cha ukoloni leo katika kijiji cha Kinole na kurejeshwa hivi karibuni katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Morogoro wa kwanza kulia ni Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt Harrison Mwakyembe.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt.Harrison Mwakyembe (wa kwanza kulia) akishuhudia baadhi ya  zana  za jadi zilizokuwa zimepotea kwa zaidi ya miaka mia moja  na kurejeshwa  hivi  karibuni zikionyeshwa  kwa jamii ya Waluguru (hawapo pichani) na Mjukuu wa Chifu Kingalu Bw.Hamis Athumani leo wakati wa sherehe za makabidhiano ya zana hizo  zilizofanyika katika himaya ya chifu huyo katika kijiji cha Kinole Kata ya Mtamba Mkoani Morogoro.
Chifu Kingalu Mwanabanzi wa XV akitoa maelezo kuhusu sanamu hiyo iliyoko  kulia kwakwe kuwa ni mfano wa mama mzazi wa  Chifu Kingalu wa Kwanza na alieleza kuwa sanamu hiyo inanguvu nyingi ikiwa ni pamoja na uwezo wa  kuzungumza na pia ni moja ya zana hizo zilizokuwa zimeibiwa na kurejeshwa, wakati wa sherehe ya makabidhiano ya zana hizo leo katika kijiji cha Kinole Mkoani Morogoro.

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt.Harrison Mwakyembe akisimikwa na  Chifu Kingalu Mwanabanzi wa XV, kuwa Chifu Mkazi miongoni mwa Machifu wa Baraza lake leo wakati wa hafla ya makabidhiano ya zana za Kijadi za Chifu huyo zilizokuwa zimepotea kwa zaidi ya miaka mia moja iliyofanyika leo katika kijiji cha Kinole Mkoani Morogoro. 
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt.Harrison Mwakyembe (wanne kulia) na Chifu Kingalu Mwanabanzi wa XV (wanne kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa baraza la chifu huyo mara baada ya sherehe za makabidhiano ya zana za kijadi ziizokuwa zimepotea kwa zaidi ya miaka mia moja na kurejeshwa hivi karibuni, ambapo sherehe hizo zimefanyika leo katika Kijiji cha Kinole Mkoani Morogoro , (watatu kulia) ni Kaimu Mkuu wa Mkoa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Ulanga Mhe.Ngollo Malenya.


Na. Anitha Jonas – WHUSM,Kinole.Morogoro.
Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Mheshimiwa Dkt.Harrison Mwakyembe ameigiza  Kurugenzi  ya Idara ya Utamaduni katika Wizara yake kufika katika himaya ya Chifu Kingalu Mwanabanzi wa XV (kumi na tano) wiki ijayo kwa ajili ya kukusanya taarifa zote zinahusu urithi wa utamaduni huo usiyoshikika wenye histori ya zaidi ya miaka mia nne iliyopita.

Mheshimiwa Dkt.Mwakyembe ameyasema hayo leo katika Kijiji cha Kinole Kata ya Mtamba Mkoani Morogoro katika hafla ya Makabidhiano ya Mali Kale za Chifu Kingalu Mwana Msumi wa kwanza wa kuanzia mwaka 1600 ambaye zana zake za jadi ziliibiwa na katika mazingira ya kutatanisha na kurushishwa hivi karibuni.

“Kwa historia ya uongozi huu wa kijadi wenye zaidi ya miaka mia nne kama nilivyoelezwa hapa na kuonyeshwa baadhi ya vitu  ninaona kuna kila sababu ya himaya hii ya Chifu kujengwa sehemu ya Makumbusho na taarifa zitakazo kuja kuchukuliwa na watendaji wangu wa wizara  nitazisimamia na  kuzipeleka katika mashirika mbalimbali ya Kimataifa ambayo yako tayari kufanya kazi na sisi na kuhifadhi  zana hizi za asili,”alisema Mhe.Dkt.Mwakyembe.

Akiendelea kuzungumza katika hafla hiyo Waziri huyo mwanye dhamana na masuala ya utamaduni alitoa wito kwa viongozi wote wa kijadi nchini kuhakikisha wanakuwa mbele katika kulinda na kuhifadhi misitu na mali kale kwani ndiyo urithi wa utamaduni kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kuongeza chachu ya utalii wa kiutamaduni.

Naye Mmoja wa Dada wa Chifu Kingalu Bibi.Gaudensia Lukwele aliyesoma risala kwa niaba ya Chifu Kingalu XV alitoa ombi kwa Wizara hiyo yenye dhamana na masuala ya Utamaduni  kuanza kutambua na kuweka katika rejesta ya wizara machifu wa Tanzania  na mali kale zao pamoja na ujuzi wa asili wa jamii zao katika makarama mbalimbali.

“Tunaomba serikali itambue na kuiwezesha miliki  ya Chifu Kingalu iwe sehemu ya makumbusho itakayo tembelewa na watu wa ndani na nje ya nchi kukidhi haja ya uchifu ikiwa ni pamoja na kuboresha miundombinu ya barabara iliiweze kufikika kwa urahisi na miliki hii niya kuvutia na ya kipekee duniani na isiyohamishika,’’alisema Bibi.Lukwele kwa niaba ya chifu.

Pamoja na hayo nae Mjukuu wa Chifu Kingalu Mwanamfuko wa Kumi Bw.Semeni Kingalu alieleza kuwa zana hizo za matambiko ya asili ya Chifu Kingalu zinauhusiano mkubwa wa kiutamaduni  baina ya nguvu za kimila na uhifadhi wa mazingira,ikiwemo uhifadhi wa misitu na uoto wa asili,vyanzo vya maji,hali ya hewa ,mvua na utajiri.

“Zana hizo zinatambulika kwa majina ,uhalisia wake na ikiwemo kumuenzi kiongozi wa kwanza Chifu Kingalu ambaye hajafa mpaka sasa hivi mwenye zaidi ya miaka mia nne na uongozi wake wa kimila upo katika mikoa ya Morogoro,Tanga,Pwani na Dar es Salaam,”alisema Mjukuu wa Chifu Kingalu.

Hata hivyo katika hafla hiyo viongozi hao wa jamii ya kichifu walisisitiza suala la jamii ya watanzania kudumisha mila asilia za makabila ya kiafrika kuziheshimu kwa kutokuwa na mmomonyoko wa maadili pamoja na desturi za kijadi zenye misingi ya amani,umoja,mshikamano,kuheshimiana na utunzaji wa mazingira.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.