WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy
Mwalimu na Mbunge wa Viti Maalumu(CCM) Mkoani Tanga kulia akizundua
jiwe la la Msingi kwenye madarasa sita ya shule ya Msingi Mwakidila
Jijini Tanga yaliyofadhiliwa na Ubalozi wa Japani nchini kutokana na
jitihada zake kuhakikisha changamoto za uhaba wa vyumba vya madarasa
vinakwisha kwenye Jiji hilo kwa kushirikiana na wadau na wananchi.
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy
Mwalimu na Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoani Tanga kulia akipiga
makofi mara baada ya kuzoindua Jiwe Msingi kwenye madarasa sita ya
shule ya Msingi Mwakidila Jijini Tanga
yaliyofadhiliwa na Ubalozi wa Japani nchini kutokana na jitihada zake
kuhakikisha changamoto za uhaba wa vyumba vya madarasa vinakwisha kwenye
Jiji hilo kwa kushirikiana na wadau na wananchi.
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu
na Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Tanga akizungumza wakati
wa hafla ya uzinduzi wa Jiwe la Msingi kwenye madarasa sita ya shule
ya Msingi Mwakidila Jijini Tanga
yaliyofadhiliwa na Ubalozi wa Japani nchini kutokana na jitihada zake
kuhakikisha changamoto za uhaba wa vyumba vya madarasa vinakwisha kwenye
Jiji hilo kwa kushirikiana na wadau na wananchi kulia ni Mkuu wa
wilaya ya Tanga.
Mkurugenzi wa Shirika la Tawode Fatuma Mganga akitoa hotuba yake
kwenye uwekaji wa Jiwe la Msingi kwenye madarasa hayo
Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza katika
halfa hiyo
Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga (DAS) Faidha Salim akizungumza
Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji akizungumza |
Naibu Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Mohamed Haniu akizungumza
Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Mwakidila akisoma risala kwa
mgeni rasmi
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy
Mwalimu na Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Tanga akisalimiana na
wataalamu mbalimbali wa halmashauri ya Jiji la Tanga wakati
alipowasili shuleni hapo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias
Mwilapwa
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy
Mwalimu na Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Tanga kushoto
akitazama madawati yaliyopo kwenye moja ya darasa ambalo limejengwa
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy
Mwalimu na Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Tanga kushoto
akitazama madarasa hayo katikati ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias
Mwilapwa
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy
Mwalimu na Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Tanga akisalimiana na
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally
Mwakababu wakati wa halfa hiyo katikati ni Mkuu wa wilaya ya Tanga
Thobias Mwilapwa kulia ni Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha
Salim
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy
Mwalimu na Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Tanga akifurahia jambo
na wanafunzi wa shule ya Msingi Mwakidila Jijini Tanga
Viongozi mbalimbali wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Waziri wa
Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu na
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Tanga
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu na
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Tanga katikati akiwa kwenye piucha
ya pamoja na viongozi mbalimbali na wanafunzi wa shule ya Msingi
Mwakidila kulia ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kushoto ni
Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy
Mwalimu na Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Tanga katikati akiwa
kwenye piucha ya pamoja na viongozi mbalimbali na wanafunzi wa shule
ya Msingi Mwakidila kulia ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi
Mayeji kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu na
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Tanga katikati akiwa kwenye picha
ya pamoja na viongozi mbalimbali na kwenye shule ya Msingi
Mwakidila kulia ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji
kushoto ni Naibu Meya wa Jiji la Tanga Mohamed Haniu
Muonekano wa madarasa sita yaliyojengwa kwenye shule ya Msingi
Mwakidila Jijini Tanga
Muonekano wa madarasa sita yaliyojengwa kwenye shule ya Msingi
Mwakidila Jijini Tanga
Muonekano wa madarasa sita yaliyojengwa kwenye shule ya Msingi
Mwakidila Jijini Tanga
Sehemu ya wananchi wa Mwakidila wakifuatilia hotuba ya mgeni
rasmi Waziri Ummy Mwalimu
Sehemu ya wananchi wa Mwakidila wakifuatilia hotuba ya mgeni
rasmi Waziri Ummy Mwalimu
Sehemu ya wananchi wa Mwakidila wakifuatilia hotuba ya mgeni
rasmi Waziri Ummy Mwalimu
Wanafunzi wa shule ya Msingi Mwakidila wakicheza wimbo wakati wa halfa hiyo |
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee wa Watoto na Mbunge wa
Viti Maalumu Mkoani Tanga Ummy Mwalimu leo ameweka jiwe la
Msingi kwenye madarasa sita shule ya Msingi Mwakidila Jijini
Tanga yaliyofadhiliwa na Ubalozi wa Japani nchini.
Ujenzi wa madarasa hayo unatokana na jitihada kubwa zilizofanywa na
Waziri Ummy kuhakikisha anashirikiana na wananchi wa Jiji la Tanga
kuweza kuzipatia ufumbuzi changamoto zinazoikabili sekta ya
elimu ikiwemo ujenzi wa madarasa kwa shule zenye uhaba ili
kuwawezesha wanafunzi kusoma bila kuwepo kwa vikwazo.
Mradi wa ujenzi huo uliofadhiliwa na Ubalozi wa Japani nchini
Tanzania kupitia shirika la TAWODE (Tanga Women Development
Initiative) una thamani ya shilingi Milioni 179,777,898.00
pamoja na madawati 180 mpaka kumalika kwake.
Akizungumza
katika halfa hiyo Waziri Ummy alisema baada ya kuwepo kwa uhaba
wa vyumba vya madarasa ambapo darasa moja kwenye shule hiyo
lilikuwa likikaa wanafunzi 166 ndipo alipoamua kuweza
kuishughulikia changamoto hiyo kwa vitendo na kufanikiwa kupata
ufadhili huo ambao umewezesha ujenzi huo.
Halfa hiyo
ilihudhuriwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa,Naibu Meya wa
Jiji la Tanga Mohamed Haniue,madiwani na viongozi
mbalimbali wakiwemo wa idara ya Elimu Jiji hilo wakiwemo
viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Tanga
wananchi,walimu na wanafunzi.
Alisema kwa serikali ya
awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli inastahili kupongeza
kila wakati kutokana na kuanzisha sera ya elimu bure ambayo
matokeo yake yameanza kuonekana kutokana na kuwepo kwa ongezeko
la uandikishaji wa wanafunzi wanaoingia darasa la kwanza Jijini
Tanga mwaka huu.
“Kwa mujibu wa takwimu za Jiji la
Tanga uandikishaji wa wanafunzi wa shule ya Msingi umeongezeka
kutoka mwaka 2015 watoto 8495 hadi watoto 10345 mwaka 2018 na
ongezeko hilo sio kwa sababu watu wanazaa sana kutokana na kwa
mujibu wa takwimu zao kiwango cha wanawake kuzaa watoto kimepungua
sana kuliko zamani mwanamke anaweza kuzaa watoto mpaka saba.
Alisema kwamba kwa sasa mwananke mmoja anaweza kuzaa watoto
kati ya watano na hao walikuwa majumbani na walikuwa hawaendi
shule kutokana na kukwamishwa na ada na michango mbalimbali
ambayo awamu hii imeamua kuiondoa na hivyo wananchi kuweza
kuwapeleka watoto wao shuleni kutokana na sera ya elimu bure
bila malipo.
Aidha aliwataka wananchi wa mkoa wa Tanga
kuendelea kumuunga mkono Rais Magufuli ili aweze kuendelea
kuijenga Tanzania mpya ya viwanda kwa vitendo kutokana na kazi
kubwa anayoifanya kuhakikisha watanzania wanapata maendeleo
“Ndugu zangu wana Tanga Rais wetu Mh Dkt John Mgufuli
amefanya kazi kubwa sana kuhakikisha watoto wanapata elimu na
kila mwezi amekuwa akitoa milioni 54 kwa shule za msingi Jiji la Tanga
na Milioni 55 kwa shule za Sekondari kwa ajili ya kuhakikisha
watoto wanasoma bila malipo hivyo niwaambieni tutamlipa kwa kazi
kubwa na mazuri kutokana na mambo makubwa aliyoyafanya
tumuonyeshe kwa vitendo kwenye serikali za mitaa kwamba tupo
pamoja naye”Alisema Waziri Ummy.
Naye kwa upande
wake Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji alipongeza juhudi
kubwa zinazofanywa na Waziri Ummy ambako kwa Jiji hilo
wanajivunia sana kuwa na kiongozi kama yeye kutokana na namna
alivyojitoa kusaidia maendeleo huku akimuhaidi kuchangia tiles
kwa madarasa hayo sita.
Alisema kwa kipindi cha mwaka 2018
waliandikisha wanafunzi darasa la kwanza asilimia 121 ya lengo
ambalo walikadiria kuandikisha akwani walikaadiria wanafunzi
8506 na waliweza kuandikisha10345 hali inayonyesha mwitiko
mkubwa wananchi kuwapeleka waoto shule.
Alisema hali
hiyo miaka ya nyuma hakuwepo huku akieleza mwitikio huo wananchi
watahakikisha wanaweka miundombinu sambamba na watoto
wanaondikishwa kwenye shule hizo ili waweze kupata sehemu ya
kusomea.
Hata hivyo alitoa wito kwa wazazi na wananchi
kushirikiana na serikali kujenga miundombinu ya shule ili kuweza
kuhakikisha wanafunzi wanaondikishwa kujiunga na darasa la
kwanza wanapata fursa ya kusoma
“Lakini pia nimshukuru
Rais kwa kuleta mpango wa elimu bila malipo kwani kwa kipindi
cha miaka miwili shule za msingi zimepokea milioni 984.8 kama ruzuku
inayokwenda moja kwa moja kwa shule kutekeleza mpango elimu bila
malipo…2017/2018 milioni 656.8 ziliwekwenda moja kwa moja shule za
msingi na mwaka 2018/2019 wamepokea kuanzia desemba milioni 325
mpango huu umeweza kuwasaidia shule zao kwenye mambo mengi
“Alisema.
Pia alisifu jitihada kubwa zinazofanywa na Waziri Ummy
kuhakikisha anakuwa mstariu wa mbele kutatua changamoto za
wananchi licha na kuwa na majukumu makubwa lakini umekuwa akitujali
watu wa Tang.
Mkurugenzi huyo alisema katika Jij la Tanga
kuna shule za msingi 104 za serikali 79 changamoto nyingi za
hali ya miundombinu shule za msingi za Jiji la Tanga mahitaji ya
vyumba vya madarasa 1251 lakini vilivyopo 710 upungufu ni vyumba
541.
No comments:
Post a Comment