Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Uongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) ukiongozwa na Makamu Mwenyekiti UWT.Bi.Thuwaiba Editon Kisasi,wakiwa katika ukumbi wa Ikulu wakiwa katika mazungumzo hayo.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein amepongeza azma ya
Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), kufanya Kongamano la Kitaifa la kupongeza
utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)kwa kipindi cha
miaka 3 ya uongozi wake.
Hayo aliyasema leo
wakati alipokutana na uongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wakiwemo
Wajumbe wa Kamati Tekelezaji ya Umoja huo Ikulu mjini Zanzibar ambapo Rais Dk.
Shein alitumia fursa hiyo kupongeza rai na azma hiyo ya Umoja huo wa (UWT).
Katika maelezo yake
Rais Dk. Shein ambaye pia, ni Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Zanzibar alieleza kuwa Kongamano hilo litatoa mwanga katika kutambua juhudi
zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika
kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020.
Rais Dk. Shein
alieleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar bado inaendelea kutekeleza
majukumu yake ambayo ni pamoja na kuimarisha miradi ya maendeleo Unguja na
Pemba, mjini na Vijijini kwa manufaa ya wananchi wote ikiwa ni miongoni mwa
utekelezaji wa Ilani hiyo ya CCM.
Hivyo, Rais Dk. Shein
alitumia fursa hiyo kuupongeza Umoja huo kwa kufikiria kufanya jambo hilo
muhimu ambalo litatoa taswira nzuri kwa jamii ambayo inatambua juhudi
zinazochukuliwa na Serikali yao katika kuwaletea maendeleo endelevu.
Aidha, Rais Dk. Shein alipongeza
kwa maandalizi ya Kongamano hilo ambalo litaanzia Kisiwani Pemba na baadae
kufanyika Unguja huku akisisitiza haja ya kuendelea kuungwa mkono Jumuiya hiyo ili
izidi kuimarika na kuleta mafanikio kwa Taifa.
Sambamba na hayo, Rais
Dk. Shein alisisitiza haja ya kuendelezwa kwa umoja na mshikamano ndani ya
Jumuiya hiyo ambayo imeweza kupata mafanikio makubwa na kuimarika zaidi tokea
kuanzishwa kwake.
Nao ungozi wa Jumuiya
ya (UWT) ukiongozwa na Makamo Mwenyekiti wake Thuwaiba Edington Kisasi ulieleza
azma na malengo ya Kongamano la Kitaifa
la kumpongeza Rais Dk. Shein kwa kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa
kipindi cha miaka 3 pamoja na kutangaza yale yote yaliyoyomo ndani ya Ilanin
hiyo ya mwaka 2015-2020.
Makamu Mwenyekiti huyo
alieleza kuwa Rais Dk. Shein ametekeleza vyema Ilani ya Uchaguzi katika uongozi
wake tena kwa kiwango kikubwa Mjini na
Vijini katika nyanja mbali mbali hivyo, kuna kila sababu ya kuendelea
kumpongeza kutokana na juhudi zake hizo ambazo ni za mfano.
Katika maelezo yake
Kisasi alieleza kuwa Kongamano hilo linatarajiwa kufanyika tarehe 9 Machi 2019
kwa upande wa Pemba na tarehe 16 Machi 2019 kwa upande wa Unguja ambalo
litawashirikisha kikamilifu akina mama.
Alieleza kuwa Kamati
ya kufanikisha Kongamano hilo inaongozwa na Mwenyekiiti wake Mgeni Hassan Juma
Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi pamoja na Wajumbe wengine.
Aidha, Makamu huyo
Mwenyekiti wa (UWT), alieleza kuwa Makongamano hayo yote yatakayofanyika Unguja
na Pemba yataambatana na ziara maalum za viongozi hao wa Jumuiya hiyo katika
Mikoa yote ya Zanzibar.
Sambamba na hayo,
uongozi huo wa (UWT), ulimueleza Rais Dk. Shein mikakati iliyoiweka katika
kuhakikisha wanafanikisha Makongamano hayo wakatayofanya Unguja na Pemba ikiwa
ni pamoja na ziara wanazotarajia kuzifanya.
Viongozi hao walitumia
fursa hiyo kuendelea kumpongeza Rais Dk. Shein kwa kuendelea kuujali na
kuuthamini Umoja huo sambamba na kuendelea kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM
ya mwaka 2015-2020 kwa vitendo.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment