Habari za Punde

ASKARI WA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI MIKOA YA KANDA YA KASKAZINI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WALEDI

Mwenyekiti wa kikao kazi ,Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Arusha Mrakibu Kennedy Komba akizungumza wakati akifungua kikao kazi leo Jijini Tanga kulia ni Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoani Tanga Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto Goodluck Zelote
 Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoani Tanga Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto Goodluck Zelote akizungumza wakati wa kikao hicho kushoto ni  Mwenyekiti wa kikao kazi ,Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Arusha Mrakibu Kenedy Komb
 Mkaguzi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Tanga Yusuph Msuya akijitambulisha wakati wa kikao hicho
 Sehemu ya wakaguzi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kutoka mikoa ya Kanda ya Kaskazini wakifuatilia kikao hicho
meza kuu wakifuatilia hoja  mbalimbali kwenye kikao hicho
 Sehemu ya Askari wa Jeshi la Zimamoto wakifuatilia kikao hicho

ASKARI wa Jeshi la Zimamoto na Ukoaji mikoa ya Kanda ya Kaskazini wametakiwa kufanya kazi kwa waledi,uaminifu na juhudi kubwa wanapokwenda kuzima moto kwa wananchi ili kuweza kuokoa mali zao na maisha hivyo kuleta matumaini mapana kwao na jamii zinazowazunguka.

Hayo yalisemwa leo na Mwenyekiti wa kikao kazi ,Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Arusha Mrakibu Kenedy Komba kwa Makamanda wa Jeshi hilo mikoa ya kanda ya Kaskazini kilichokuwa na lengo la kubadilisha uzoefu na kuona namna ya kutekeleza shughuli zao kwa ufanisi mkubwa katika kutoa huduma kwa wananchi wa mikoa hiyo.

Alisema anamina baada ya kumalizika kwa kikao hicho kila Kamanda na mkuu wa kitengo atakuwa amepata faida na kuleta matokeo yaliyomema na kutukuka kwenye kutoa huduma kwa watanzania mikoa wanayotoka na Taifa kwa ujumla.

Alisema dhamira kubwa hivi sasa kwao ni kuhakikisha wanaendelea kutoa elimu kwa wananchi waweze kujua kazi wanayoifanyika hususani wanapokwenda kuzima moto hivyo wategemee maokozi yatafanyika kwa juhudi kubwa yawe ya mali au wananchi ili kuleta matumaini mapana kwa wananchi.

Komba alisema katika kila kazi inapoifanya kwenye sehemu ya kazi kunapaswa kufanya kazi kwa uaminifu na waledi ili kuwafanya waananchi wawweze kuwaamini katika utekelezaji wa shughuli zao za kila siku kupambana na majanga ya moto

“Suala kubwa ni uaminifu na ueledi kwenye kutekeleza majukumu yetu na tusipofanya hivyo tutapoteza imani kwa weananchi ...tujenge mahusiano mema na wananchi lakini kubwa zaidi kutekeleza majukumu kwa ufanisi mkubwa ambao utasaidia kupata wadau walio wema wenye hiari ya kutusaidia kutupa mawazo kwa sababu ya waledi tunaoufanya “Alisema

“Kila mkoa kuchukua yale mazuri yatakayowasilishwa kwenye kikao hicho kwenda kuyafanyia kazi ili kikao kijacho kila mkoa uweze kuleta mafanikiona sio malalamiko kwa kufanya hivyo Jeshi litakuwa la mfano na kuleta matokeo changa kwa mkoa na Taifa kwa ujumla”Alisema

Alisema hatua hiyo ya kukatana na kubadilisha uwezo wa kazi zao wanazofanya italeta matokeo changa kwa wananchi wanao wahudumia kwenye mikoa ya Kanda ya Kaskazini.

Naye kwa upande wake Mkaguzi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Tanga Yusuph Msuya alisema dhani ya idara ya ukaguzi ni kupunguza majanga kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo kwenye majengo, magari ili kuwawezesha watumiaji kuepukana nayo.

Alisema mpaka sasa wamekwisha kufanya kwa vyombo vya moto vipatavyo 384 ambapo kati ya hivyo mabasi 235 hali zao ni nzuri na yaliyosalia tumewapa ushauri namna ya kufanya ili waweze kuondokana na mapungufu yaliyobainika.

“Ukaguzi tulioufanya kuanzia mwezi Desemba mpaka sasa kwa vyombo 384 kati ya hivyo mabasi 235 hali zao ni nzuri na yasiyosali tumewapa ushauri ili waweze kuondoa mapungufu yaliyobainika”Alisema

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.