Habari za Punde

Mama Asha mgeni rasmi katika zoezi la uchangiaji wa ujenzi wa mabweni ya Skuli ya Mlingano Sekondari mkoani Tanga

 Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi akimfariji mtoto Hassan Suleiman wakati alipowasili Wilayani Muheza ambae ni mlemavu akiwa katika kigari chake maalum.
 Vifaa mbali mbali vilivyotolewa katika shughuli ya watoto wenye Mahitaji maalum  na wadau walioguswa na watoto hao, vifaa hivyo vinajumuisha baiskeli, wll chair, pamoja na magongo kwa ajili ya kusaidia katika kutembea.
 Mama Tunu Pinda akimvisha Kofia Mtoto mwenye ulemavu wa ngozi wakati akimzawadia kupitia vifaa tofauti alivyovikabidhi kwa uongozi wa wilaya hiyo ikiwa ni sehemu ya kuwachangia watoto hao. Mama Tunu Pinda ni mwenyekiti wa wake wa viongozi Tanzania bara

 Mama Asha Suleiman Iddi Akimlisha Keki mtoto Maimuna Yahya wa skuli ya msingi ikiwa ni moja ya kuwazawadia watoto waliofanya vizuri katika masomo yao.
 Mke wa Makamu wa Pili wa Rais Mama Asha Suleiman Iddi Akihutubia wananchi waliofika katika zoezi la uchangiaji wa ujenzi wa mabweni ya Skuli ya Mlingano Sekondari kwa wototo wenye Mahitaji maalum huko Wilaya ya Muheza Mkoani Tanga

Mgeni Rasmi katika shughuli ya kuwachangia watoto wenye mahitaji maalum  Mama Asha Suleiman Iddi akimkabidhi Mhe. Mkuu wa wilaya ya Muheza Eng. Asha Tumbo Shillingi Million Sita (6,000,000/) kwa ajili ya ujenzi wa mabweni ya Wanafunzi wenye ulemavu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.