Habari za Punde

Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa Arudi CCM.

Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa akiwasili katika Ofisi ndogo za Chama cha Mapinduzi CCM Lumumba jijini Dar es Salaam kabla ya kutangaza rasmi kurejea katika Chama cha Mapinduzi CCM leo tarehe 1 Machi 2019.

 Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili katika Ofisi ndogo za Chama cha Mapinduzi CCM Lumumba jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi  CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli akishuhudia. Wakwanza kushoto ni Kada wa CCM Rostam Azizi
 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi  CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa ambaye ametangaza kurejea chama cha Mapinduzi CCM akitokea chama cha CHADEMA katika Ofisi ndogo za Chama cha Mapinduzi CCM Lumumba jijini Dar es Salaam.
 Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa akitangaza rasmi kurejea chama cha Mapinduzi CCM mbele ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi  CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu Mwenyekiti wa CCM bara Philip Mangula, Katibu wa CCM Bashiru Ally, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, pamojan na Kada wa CCM Rostam Azizi.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi  CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza kumkaribisha Waziri Mkuu mstaafu Edward Lowassa ambaye amerejea rasmi CCM.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.