Habari za Punde

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Nchini afanya mabadiliko ya baadhi ya Makamanda wa Mikoa.


                                             JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
            WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
                                        JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI

            JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI
  S. L. P. 1509,
  DODOMA.
29 Aprili, 2019

 

Simu ya maandishi: “ZIMAMOTO KUU”
Simu Nambari:  +255-22-2113537
Telefax:          + 255-22-2184569
Tovuti : www.frf.go.tz

                                                                                                   


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KAMISHNA JENERALI WA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI NCHINI AFANYA MABADILIKO YA BAADHI YA MAKAMANDA WA MIKOA

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, (CGF) Thobias Andengenye, amefanya mabadiliko ya baadhi ya Makamanda wa Mikoa hapa nchini.

Makamanda walioguswa na mabadiliko hayo ni Kamishna Msaidizi wa Zimamoto (ACF) Mohamed Kondo, aliyekuwa Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kinondoni, anaenda kuwa Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mbeya.

Kamishna Msaidizi (ACF) Juma Yange, aliyekuwa Kitengo cha Utawala Mkoa wa Kinondoni, anakuwa Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kizimamoto Kinondoni.

Mrakibu Msaidizi wa Zimamoto (ASF) John Francis, aliyekuwa Chuo cha Zimamoto na Uokoaji Handeni Mkoani Tanga, anaenda kuwa Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Rukwa.

Vilevile, aliyekuwa Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kigoma, Mrakibu Msaidizi wa Zimamoto (ASF) Athumani Basuka, anaenda kuwa Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Wilaya ya Hai – Siha, nafasi yake inachukuliwa na Mrakibu Msaidizi (ASF) Jumbe Juma.

Pia aliyekuwa Kamanda wa Kiwanja cha Ndege Mkoa wa Iringa, Mkaguzi wa Zimamoto (INSP) Hamisi Dawa, anaenda kuwa Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kagera.

Mabadiliko haya ni ya kawaida yanayotokea ndani ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, katika kuongeza ufanisi wa utendaji kazi.


Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linaendelea kutoa wito kwa Wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Makamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mikoa na Wilaya katika suala la Kinga na Tahadhari Dhidi ya majanga.
Imetolewa na;     
Joseph Mwasabeja – (INSP)
Msemaji wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
Makao Makuu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.